Home » » JELA MIAKA MITANO KWA WIZI WA NG’OMBE

JELA MIAKA MITANO KWA WIZI WA NG’OMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda imemuhukumu  John Ngasa (32) Mkazi wa Kijiji cha Mwamkulu  Wilaya ya Mpanda kutumikia  jela kifungo cha miaka mitano jela baada  ya kupatikana na hatia ya  kuiba Ng’ombe mbili  zenye thamani ya  shilingi laki mbili.
Hukumu hiyo ilitolewa hapo jana na Hakimu  mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Odira Amwol mara baada ya kulizika na ushahidi uliotolewa  Mahakamani hapo na upande wa mashitaka  uliokuwa na mashahidi watano.
Awali  katika  kesi hiyo  Mwendesha  Mashitaka  Kulwa  Kusekwa  alidai kuwa  Ngasa  alitenda kosa hilo  Aprili 25, 2015  majira ya saa   mbili  usiku huko  katika Kijiji cha Mwamkulu Wilayani Mpanda.
Siku hiyo ya  tukio mshitakiwa  anadaiwa  kukamatwa akiwa ameiba Ng’ombe  wawili wa mwanakijiji  mwenzake aitwaye Madirisha Msalaba zenye thamani ya shilingi laki tisa .
Mwendesha Mashitaka Kulwa alidai kuwa   mtuhumiwa huyo baada ya kuiba Ng’ombe hao alianza kuwaswaga kwa ajiri ya kuwapeleka eneo jingine  hata hivyo wakati akiwa  bado njiani Askari wa jadi(Sungusungu) wa Kijiji hicho walipata taarifa ya kuibiwa  kwa Ng’ombe hao na ndipo walipofanikiwa kumkamata mshitakiwa Ngasa akiwa na Ng’ombe hao wawili.
Katika utetezi wake  Ngasa  ambae hakuwa na shahidi hata mmoja  huku  upande wa mashitaka ukiwa mashahidi watano  alikana kuiba Ng’ombe hizo .
Hakimu Odira Amwol  kabla ya kusoma huku  aliiambia Mahakama  kuwa mshitakiwa amepatikana na hatia ya kuiba Ng’ombe wawili kutokana  na ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo na upande wa mashitaka  hivyo mshitakiwa anapewa nafasi  ya kujitetea kama unasababu yoyote ya msingi ya kuiomba Mahakama impunguzie adhabu .
Mshitakiwa Ngasa katika  utetezi wake aliomba Mahakama impunguzie adhabu  kwa kuwa Mama yake mzazi pamoja na wadogo zake wanamtegemea yeye .
Utetezi huo ulipigwa vikali  na Mwendesha Mashitaka Kulwa  ambae aliiomba Mahakama itowe adhabu  kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho  kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.
Hakimu  Amwol alisoma ukumu na kuiambia Mahakama kuwa  mshitakiwa  John Ngasa  amahukumiwa   na Mahakama hiyo kwenda  kutumikia jela kifungo cha miaka mitano jela kuanzia jana na kama haja lidhika na hukumu hiyo anayonafasi ya kukata rufaa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa