Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi linawashikilia watu
watatu kwa tuhuma za kuwakamata na meno ya Tembo yenye thamani ya
shilingi milioni 120 ambayo ni sawa na
Tembo wazima wanne .
Watuhumiwa hao
watatu waliokamatwa na meno hayo ya Tembo
wametajwa kuwa ni Bathromeo
Agustino(26) Geofrey Exavery(40) na Elias Mwelela( 40) wakazi wa Mtaa wa
Aitel Kata ya Uwanja wa Ndege Manispaa ya Mpansa.
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa
watuhumiwa hao walikamatwa juzi majira
ya saa nne usiku katika Mtaa huo wa Airtel waliko kuwa wakiishi.
Alisema Jeshi
la Polisi na Askari wa
(TANAPA) wa HIFADHI
ya Taifa ya mbuga ya Katavi walipatataarifa kutoka kwa Raia wema kuwa katika Mtaa huo kuna watu wanamiliki nyara za Serikali.
Kamanda
Kidavashari alieleza baada ya taarifa
hizo kuwa zimepokelewa na
ufuatiliaji ulifanyika katika makazi waliokuwa wakiishi watuhumiwa
hao watatu.
Alisema ndipo siku hiyo ya tukio upekuzi
ulipofanyika kwenye makazi ya watuhumiwa
na katika upekuzi huo watuhumiwa hao walikutwa na meno ya Tembo vipande
12 vyenye thamani ya shilingi milioni 120
ambayo ni sawa na temba wanne hai yakiwa kwenye makazi yao.
Kidavashari
aliendelea kueleza kuwa watuhumiwa mbali
ya kukamatwa na meno hayo ya Tembo pia walikutwa na mzani mmoja
na Pikipiki aina ya Sanya yenye
Namba za usajiriT.552 CZE.
Alisema
watuhumiwa wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa hatua za
upelelezi na watafikishwa Mahakamani
baada ya upelelezi utakapo kuwa
umekamilika .
Kamanda wa polisi
wa Mkoa wa Katavi ametowa onyo kwa Wananchi kuacha mara moja kujihusisha na
biashara za nyara za Serikali na biashara haramu .
0 comments:
Post a Comment