Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Watu wawili Mshaki
Mashauri(22) na Victoria Mbas(28)
wakazi wa Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamefariki Dunia baada ya kugongwa na gari wakati wakiwa wamepakizana kwenye baiskeli
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia Waandishi wa Habari jana kuwa tukio hilo lilitokea hapo jana katika
eneo la Kagera Kata ya Kibaoni
Wilaya ya Mlele majira ya saa
kumi na moja jioni
Kamanda
Kidavashari alisema ajari hiyo ya gari
ililihusisha gari No 504 CFA aina ya Toyota Rav4 iliyokuwa ikiendeshwa na
Dreva Zakaria Feliki(47) Mkazi wa Kata
ya Usevya Wilaya ya Mlele
Alisema gari hilo lilikuwa
lilikuwa likitokea katika Kijiji
cha Kibaoni likiwa linaelekea katika
Kijiji cha Usevya Tarafa ya Mpimbwe
Gari hilo lilipofika maeneo ya Kagera Kata ya Kibaoni lilimgonga mwendesha baiskeli
Mtaki Mashauri na abilia wake Victoria Mbas na kuwasababishia vifo ambapo
Mtaki alifariki hapo hapo kwenye
eneo la tukio na Victoria alifariki Dunia muda mfupi baada ya kuwa
amefikishwa Zahanati ya Kibaoni
Alisema
Dreva wa gari lilo alikamatwa na
anashikiliwa na jeshi la polisi
na gari lake limehifadhiwa katika
kituo cha polisi cha kibaoni wakati uchunguzi ukiwa bado unaendelea
Kindavashari
alieleza kuwa mili ya marehemu wote wawili
imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti
katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda
kwa ajiri ya uchunguzi
Chanzo cha ajari hiyo ilitokana na mwendo kasi wa gari ambapo dreva wa gari
hiyo alikuwa akishindani kukimbia mwendo
kasi na mwendesha pikipiki
Mtuhumiwa
anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara
baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika
ili aweze kujibu mashitaka yanayomkabili
0 comments:
Post a Comment