Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Jeshi la
Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia
Salome Makala(32) Mkazi wa Kijiji cha
Mwenge Kata ya Nsimbo Wilaya ya
Mlele Mkoani hapa kwa tuhuma ya
kuwaorodhesha majina wanakijiji
wenzake na namba za
vipalata vya kupigia kura
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari mtuhumiwa alikamatwa
hapo juzi majira ya saa nne usiku katika
Kijiji hicho cha Mwenge
Alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia
taarifa zilizotolewa kwa jeshi la Polisi
kutoka kwa mgombea ubunge wa
Jimbo la Nsimbo Gerald Kitabu(CHADEMA)
Alisema baada ya polisi kupata taarifa hizo walifika kwenye kijiji hicho na kumkuta salome akiwa na orodha ya majina ya wanakijiji wenzake na namba za
vipalata vya kupigia kura akiwa
ameandika kwenye daftari lake
Kidavashari
alisema Polisi walimkamata mtuhumiwa na kumfikisha kwenye kituo cha polisi cha Nsimbo kwa ajiri ya mahojiano
Alieleza
baada ya mahojiano mtuhumiwa alieleza
kuwa alikuwa anakusanya taarifa
za Wanachama wa umoja wa wanawake wa CCM(CWT) kwa kuwa
katika kijiji hicho cha Songambele akikuwa na kumbukumbu zozote
Kidavashari
alisema Jeshi la Polisi bado
linaendelea kumhoji mtuhumiwa Salome
Makala ili kuweza kupa ukweli zaidi wa
tukio hilo
0 comments:
Post a Comment