Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mbunge wa viti
maalumu(CHADEMA) Anastella Malack
ambae amemaliza muda wake jana
ametangaza rasmi kujiondoa CHADEMA
na kurudisha kadi ya chama hicho
na kujiunga na chama cha ACT Wazelendo na kukabidhiwa kadi ya chama cha ACT Wazalendo
Malack alirudisha
kadi hiyo hapo jana kwa kiongozi mkuu wa
chama cha ACT wazelendo
Zitto Kabwe kwenye mkutano wa
hadhara uluofanyika katika uwanja wa Kashaulili Mjini
hapa
Katika mkutano pia
aliyekuwa diwani wa Kata ya
Makanyagio (CHADEMA) I ddy Nzyiguye
alitangaza rasmi kujiunga na
chama cha ACT
baada ya kurudisha kadi ya CHADEMA na kukabidhiwa kadi ya ACT
wazelendo
Kabla ya kuwakabidhi kadi za
Chama hicho Zitto
Kabwe alipokea kadi za kutoka kwenye
vyama mbalimbali ambazo wanachama
wa vyama hivyo walimkabidhi na kasha aliwapatia kuwapatia
kadi za ACT wazalendo
Katika hotuba yake ya kuwapokea walokuwa wanachama hao na viongozi kupitia chama hicho
aliwataka viongozi wa ACT
kutozitupa kadi hizo zilizo rudishwa wala kuzichoma moto na badala
yake wazirudishe kwa makatibu wa Mikoa husika
ambako wanachama hao waliko toka
Pia aliwataka wanchi
wa Mkoa wa Katavi kuwachagua viongozi
ambao wanania ya kuleta maendeleo
kwa wananchi wao
Alisema wapo baadhi
ya watu wnataka wachaguliwe kwa manufaa
yao binafsi badala ya manufaa ya wananchi waliowachagua
Vilele
aliwaambia Wananchi hao kuwa chama
chake cha ACT wazalendo kitaweka
wagombea wa nafasi za ubunge katika majimbo yote matano ya Mkoa wa Katavi na
wagombea Udiwani katika kata zote
54 za Mkoa wa Katavi
Kwa upande wake
aliyekuwa mbunge wa Viti Maalumu
Annastela Malack aliwataka wananchi wa Mkoa wa Katavi
kushikamaene ili kuleta maendeleo katika Mkoa huo
Alisema Mikoa ya Katavi
Tabora , Kigoma na Rukwa
ipo nyumba kimaendeleo hivyo
bila kuwepo na mshikamano ya wananchi wanao ishi kwenye mikoa hiyo
maendeleo hayatakuwepo
0 comments:
Post a Comment