N a Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mwenyekiti wa Kitongoji
cha Songambele Kata ya Ilela
Tarafa Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa
Katavi (ACT) Richald Madirisha(31)
ameuwa kikatili kwa kuchinjwa shingo
na kutenganishwa na kiwiliwili
chake na kisha nyonfolewa viungo vyake
vya mikono na miguu na sehemu zake za
siri na kisha kichwa chake na viungo hivyo kupikwa ndani ya
safuria kama mboga
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari mauwaji hayo ya kikatili na kutisha
yalitokea hapo jana majira ya saa tano na nusu usiku nyumbani kwa
marehemu
Siku hiyo hiyi ya tukio marehemu alikuwa
amelala nyumbani kwake akiwa na mkewe
aitwaye Mekilina Mussa
ghafla walitokea watu watano ambao
hawafahamiki na kuvunja mlango
kisha waliingia ndani ya nyumba
Kamanda Kidavashari alisema watu hao ambao walikuwa wameshika
mapanga baada ya kuingia ndani ya nyumba
waliingia chumbani kwa marehemu na
kumlazisha mkewe ajifishe kwa kujifunika na shuka usoni na alale kitandani
Alisema
baada ya mkewe kujifunika na shoka usoni watu hao walianza kumchinja
shingo mrehemu kwa kutumia panga huku mkewe akiwa anasikia jinsi
marehemu alivyo kuwa akilia kwa uchungu
Kidavashari alieleza baada ya kuwa wamemchinja
shingo walichukua kichwa chake na
kukiweka kwenye safuria na kuweka maji ndani ya safuria na kutoka nacho nje na kupipika
kwenye moto ambao ulikuwa unawake nje ya nyumba ya marehemu
Alisema kisha watu hao walirudi ndani ya
nyumba na kunyomfoa sehemu za siri za marehemu na mikono yake na kwato za miguu kisha
waliziweka kwenye safuria jingine
na kuvipika kwenye moto
Kisha watu
hao waliondoka na kutokomea kusiko julikana huku wakiwa wameviacha viongo hivyo vya marehemu vikiwa vinaendelea
kuchemka ndani ya safuria hizo
Kidavashari alisema mke wa
marehemu baada ya kuona watu hao wametokomea alitoka nje na kwenda kutoa
taarifa kwa majirani ambao walifika kwenye eneo hilo na kukuta viongo hivyo vikiwa ninaendelea kuchemke kwenye safuria hizo huku kiwailiwili chake
kikiwa ndani ya chumba chake
Amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauwaji kimetokana na visa vya marehemu na mtu mmoja
ambae walikuwa wakiishi nae Tabora
ambae alikuwa akimtuhumu
marehemu kuwa amemnyanya mwanamke ambae walikuwa na mahusiano nae ya kimapenzi ambae marehemu
aliamua kuhama nae kijijini hapo na kuhamia nae kijiji cha
Songambele Wilaya Mlele
Kamanda Kidavashari alieleza
jeshi la polisi Mkoa wa Katavi limewakamata na linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kuhusika na mauwaji
hayo ya kikatili
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment