Home » » WANAFUNZI WA SEKONDARI WAWASHAMBULIA WANAKIJIJI WAKIWATUHUMU KUMUUWA MWALIMU WAO KWA USHIRIKINA

WANAFUNZI WA SEKONDARI WAWASHAMBULIA WANAKIJIJI WAKIWATUHUMU KUMUUWA MWALIMU WAO KWA USHIRIKINA


Na Walter Mguluchuma
Katavi
Wanafunzi  wa Sekondari  ya Usevya  Wilayani  Mlele Mkoa wa Katavi  wamezishambulia  familia mbili  kwa kutumia   silaha  za jadi na kuwavunjia nyumba  zao baada  ya kuzituhumu  familia hizo  kuwa zinajihusisha  na  vitendo  vya  kishirikina  uliopelekea kifo   cha mwalimu  wao
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi  Dhahiri Kidavashari  alisema  tukio hili  lilitokea  hapo  juzi  majira  ya  saa  12 alfajiri  baada ya wanafunzi  wa shule  hiyo walipo  pata taarifa  ya kifo  cha mwalimu  wao Tumsifu  Philimon  (28) aliye  fariki  dunia  katika Hospital ya Sumbawanga  aliko  kuwa akipatiwa matibabu  usiku  wa tukio hilo.
Kidavashari  aliwataja   walio  vamiwa  nyumba zao  na wanafunzi  kuwa  ni  Philipo  Mwanjisi  na Aprotina  Mkalala  ambapo  mbali  ya nyumba zao  kuvunjwa   walishambuliwa pia  kwa kupigwa  na mawe
Kabla ya tukio hili  mmoja  wa  familia hizo    alifika  shuleni  hapo  wiki iliyo  pita   kwa lengo  la  kuonana  na  Mwalimu Tumsifu  baada ya kupata  malalamiko  kutoka  kwa mtoto wake  aliye kuwa akisoma hapo  alikwenda  mshitaki mwalimu  huyo  kwa mzazi wake kuwa  amepingwa viboko  na mwalimu Tumsifu adhabu ambayo mzazi huyo hakuridhika nayo
Inadaiwa  baada ya mzazi huyo  kufika  shuleni  hapo  alimpa  vitisho  mwalimu  huyo  huku  baadhi ya wanafunzi  wakisikiza  vitisho vilivyo  tolewa  na mzazi  huyo  wa mwanafunzi
Siku  iliyo fuata  mwalimu  huyo  aliamka  akiwa anaumwa   na ndipo  alipo  amua  kusafiri  hadi  Sumbawanga  waliko  wazazi  wake kwa lengo  la kwenda  kupata matibabu
Ilipofikia April 12  mwalimu huyo alitoweka hospital hadi hapo april 15 ambapo mwili wake uliokotwa akiwa amekufa kando kando ya mto huku akiwa amenyofolewa macho
Kamanda  Kidavashari  alisema   wanafunzi   hao  walihisi  kuwa kifo   cha  mwalimu  wao   kimesababishwa  na kurogwa  na wanakijiji hao  wawili  nandipo  walipo amua  kwenda  kushambulia    wanakijiji hao  na kuvamia nyumba    zao
Alisema upelelezi wa tukio hili  unaendelea  ili kuwabaini  wanafunzi  wote  walio husika  na tikio  hilo  na   watakao bainika waweze kuchukuliwa  hatua
Kwa upande  wake  mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanali Gemela Rubinga alisema  anategemea  leo  kwenda  shuleni hapo ili kuzungumza  na wanafunzi hao  wa shule  ya Sekondari ya Usevya  ili kubaini   chanzo  cha  vurugu  hizo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa