Home » » WAWILI WASHIKILIWA NA POLISI KWA KUWAZUIA ASKARI MAGEREZA WASIFANYE KAZI YAO

WAWILI WASHIKILIWA NA POLISI KWA KUWAZUIA ASKARI MAGEREZA WASIFANYE KAZI YAO


Na Walter Mguluchuam
Sumbawanga.
JESHI la polisi Mkoani Rukwa  linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuzuia askari magereza kufanya kazi ya kumkamata  Mfungwa aliyetoroka katika gereza za mahabusu la Sumbawanga ,aliyekuwa akitumikia kifungo cha miaka 15 jela baada ya kupatikana na hatia ya unganganyi wa kutumia silaha.
Aidha katika tukio hilo askari wa magereza walimjeruhi kwa risasi  kijana Isiaka  Andrea mwenye(17) ambaye ni mdogo wa mfungwa  aitwae Nizal Paschal alitoroka  kifungo chake mwaka mmoja uliopita baada ya kutumikia kifungo cha mwaka mmoja gerezani .
Akizungumza na vyombo vya  habari kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa Bw Jacob Mwaruanda amesema kuwa tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika kijiji cha Isesa  kilichopo katika manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa, na kuwataja vijana hao wanaoshikiliwa na jeshi hilo kuwa ni Mosea Andrea(19),Pamoja na Nduguye aitwae Isiaka  Andrea(17) ambaye amelazwa ward namba tatu  ya hospitali ya mkoa  wa rukwa akitibiwa jeraha la risasi lililopo katika mguu wake wa kulia
Akifafanua juu ya tukio hilo kamanda Mwaruanda amesema kuwa inadaiwa  kuwa askari hao waliizingira nyumba hiyo mara baada ya kupata taarifa za siri toka kwa raia wema zilizoeleza kuwa mfungwa aliyetoroka gerezani mwaka mmoja uliopota amerudi na kuungana na familia yake na ndipo siku ya tukio majira ya jioni askari hao wa magereza walifika katika nyumba hiyo kwa lengo la kumkamata kijana huyo ili sheria iweze kuchukua mkono wake.
Alisema kuwa hata hivyo mara baada ya kufika katika nyumba hiyo ndipo vijana hao pamoja na nduguyao ambaye alifanikiwa kutoroka  mara baada yaa kugundua kuwa waliopo nje ya nyumba yao ni askari walitoka wakiwa na silaha za jadi mikononi mwao kwa lengo la kutaka kuwajeruhi askari hao na kwa bahati nzuri askari mmoja alifyatua risasi iliyomjeruhi kijana huyo mguuni.
Kamanda Mwaruanda alisema kuwa mara baada ya vijana hao kuona askari hao wametumia silaha hiyo ndipo walipotupa silaha zao za jadi ambazo ni mapanga mishare na marungu jambo lililofanikisha askari hao kuwakamata huku mfungwa aliyetoroka gerezani akifanikiwa kuwakacha askari hao
Kwa upande wake baba mzazi wa mfungwa huyo aliyetoroka na kusababisha kizazaa kwa familia yake Bw Paschal Andrea  amesema kuwa  majira ya saa sita usiku nyumba yake ilivamiwa na askari magereza saba ambao kwa usiku huo hakuweza kutambua kuwa ni askari kutokanaa na kiza kinene kutanda ,na kisha askari hao  bila ya kufuata taratibu na kufyatua risasi iliyomjeruhi kijana wake,
Alisema kuwa mara baada ya kijana wake kujeruhiwa alianza kupiga kelele za kuomba msaada ndipo mzee huyo ambaye alikuwa amelala  na kuamshwa kwa kelele za risasi alipotoka  na kisha nae kuambulia kipigo toka kwa wajela hao ambao alifanikiwa kuwatoroka muda mfupi baadaye.
Naye Mwenyekiti wa kijiji hicho cha Isesa   Bw Revocatus Kasuku  licha ya kulaani  kitendo hicho cha kijana huyo kujeruhiwa kwa risasi amesema kuwa kwa kipndi kirefu sasa  watumishi wa jeshi  la polisi wamekuwa wakifika katika kijiji hicho na kuendelea na oparesheni mbalimbali bila ya kuwashirikisha w viongozi wa maeneo hayo.
Bw Kasuku amesme kuwa kutokana na vitendo hivyo kuendelea kwa muda mrefu sasa amekwisha peleka barua ya malalamiko kwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya sumbawanga ambaye ni mkuu wa wilaya hiyo na anasubiri utekelezaji wake.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa