Home » » WATU WAWILI WAUAWA KWA WIZI WA MBUZI

WATU WAWILI WAUAWA KWA WIZI WA MBUZI

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Watu wawili   wakazi wa  kijiji  cha Matandalani   wilaya ya mlele Mkoa  wa Katavi  wameuwawa na wananchi   baada ya kukili kuiba mbuzi  dume  wa  mwanakijiji  mwenzao
Kamanda wa  Polisi  wa Mkoa  wa  Katavi Dhahiri Kidavashari  aliwataja walio uwawa  kuwa   ni Alex Kazimoto (28) Tonora Luchagula (30)  wote wakazi  wa kijiji   cha Matandalani
Alisema tukio hili  lilitokea  Aprili  14 mwaka huu majira  ya saa saba  mchana ambapo  chanzo  cha  vifo  vya watu hao  vilitokana  na wizi  wa mbuzi  walioiba  hapo  Aprili 10  nyumbani  kwa  Jacob Sekela
Jacob baada ya kugundua  mbuzi  wake dume  ameibiwa  alikwenda  kutoa taarifa  kwa mwenyekiti wa  kijiji  hicho Malcus Wimbi  ambae  nae  aliwapa  jukumu askari   mgambo wa kijiji  hicho  kumtafuta mbuzi   huyo aliye ibiwa
Kamanda Kidavashari  alieleza  ndipo  askari mgambo  walimkamata Tonora Luchagula  na walipo muhoji alikiri  kuiba mbuzi  huyo akiwa  na  marehemu   Alex Kazimoto  na ndipo  mgambo  hao  walipo  wachukua  watuhumiwa   na kuwapeleka  nyumbani  kwa mwenyekiti
Ndipo ilipo timia  saa 2 usiku kundi la  watu lililo jiita Mwano  lilifika  nyumbani  kwa mwenyekiti  na kumwamuru  mwenyekiti awape watuhumiwa  hao  baada  ya   mwenyekiti  kuwakatalia  walianza kumshambulia  na kufanikiwa   kuwatoa watuhumiwa   na kuondoka nao   na walimuonya mwenyekiti asiwafuate  vinginevyo  watamuuwa
Kamanda  alisema  kundi hilo   lilikwenda na watuhumiwa hadi nyumbani  kwa  Donard  Sorera  ambae  ndie  anadaiwa kuwa  ndiye aliye  watuma  kwenda kuiba mbuzi  huoyo walipo mkosa  ndipo  walipoanza  kuwashambulia  wahuhumiwa  kwa kutumia  silaha za jadi   hadi  kufa
Katika tukio hilo  watu  wawili  Deus Zegula  na Malcus Wimbi  wanashikiliwa  na jeshi  la polisi  kuhusiana na   mauwaji  ya watu  hao kwa ajiri  ya maojiano
Jeshi  la polisi mkoa wa Katavi   limetoa wito  kwa wananchi  kutojichukulia  sheria mikononi  na badala yake  watowe ushirikiano  kwa jeshi hilo  kwa kutowa taarifa  ambazo  zitaweza  kuwabaini  watuhumiwa  wanao husika  na matukio  kama haya  ili waweze kukamatwa  na kufikishwa  mbele  ya vyombo   vya dora  na sheria  iweze kuchukua  mkondo wake

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa