Home » » KIJANA WA MIAKA 26 JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA KIKONGWE

KIJANA WA MIAKA 26 JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA KIKONGWE

Na Walter Mguluchuma
Mpanda
Mahakama  ya Hakimu mkazi ya Wilaya  ya  Mpanda Mkoa  wa Katavi   imehukumu Sindembala Msagi  (26) mkazi  wa  kijiji   cha Bulembo  ya wakimbizi   ya Katumba   wilaya  ya Mlele  kifungo   cha miaka  30 jela   kwa  kosa  la kumbaka  kikongwe  mwenye  umri wa miaka( 90)
Hukumu  hiyo  ilitolewa  jana  na  Hakimu  Mkazi  Mfawidhi  wa  mahakama ya   wilaya   ya Mpanda  Chiganga  Tengwa  baada  ya kulidhika  na  ushahidi  ulio  tolewa  mahamani  hapo  na  pande   wa mashitaka  na utetezi
Awali katika  kesi hii  mwendesha  mashitaka    wa  jeshi  la  polisi  Inspekita  msaidizi Ally Mbwijo  alidai mahamani  hapo  kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo  Desemba  23 mwaka  jana  nyumbani  kwa kikongwe huyo  aliye  kuwa  ana   tatizo la ugonjwa  wa kupoza  mguu na mkono wa kushoto
Mshitakiwa  Sindembala  alidaiwa  siku  hiyo majira  ya saa tano usiku  alikwenda  nyumbani  kwa mama huyo aliye kuwa akiishi  peke yake  na kubomoa mlango  wa nyumba  ya mama huyo   na kisha kuingia ndani
Mwandesha  mashitaka  alieleza  mshitakiwa  baada  ya  kuingia ndani  alimshika  kwa nguvu  kikongwe  huyo  na kuanza kumbaka licha ya mama  huyo kupiga  mayowe  hakuweza  kupata msaada  kwa majirani  kutokana  nyumba  ya mama huyo  kuwa mbali na majirani wenzake
Kikongwe  huyo  alijaribu  kumsihi  mshitakiwa  afimfanyie kitendo  hicho  kutokana  na umri   wa mama huyo  kuwa mkubwa  na tendo hilo alisha liacha  miaka mingi iliyo pita
Alisema mahamani hapo  mshitakiwa  Sindembala  aliombwa na mama huyo  amwache  kumbaka  na akawatafute wanawake  wanao lingana   nae  lakini  mshitakiwa aliendelea  kumbaka   kikongwe bila kujari  uzee wake
Mwandesha mashitaka Ally  Mbwijo  aliendelea  kueleza  mshitakiwa   baada ya  kumbaka  mama huyo  kwa muda mrefu  alijikuta amechoka   na kupatwa  na  usingizi  ulio mfanya  alale  ndani ya chumba cha kikongwe
Ilipo  timia  muda  wa saa 12 alfajiri  mama  huyo alifungua  dirisha  na kumwona mtu mmoja akipita aitwaye Abushola Elly jirani na nyumba  yake  ndipo   alipo mwita kwa ishara  ya vidole  na mtu huyo aliweza  kuitikia wito na  mama huyo  alimwoleza kuwa amebakwa   na aliye mbaka   bado  yumo  ndani  amesinzia
Mtu huyo  ambae alikuwa shahidi katika  kesi hii aliingia  ndani  na kumkuta  mshitakiwa akiwa bado amelela  na baada ya kuwa amemtambua   aliogopa kumkamata  akiwa peke  yake  kutokana  na tabia  aliyo  kuwa nayo   mshitakiwa  Sindembula  ya ukorofi na ugomvi   hari ilyo mfanya akimbie kwende  kuwaita majirani
Mwendesha mashitaka  alieleza   majirani  walipo fika  katika eneo hilo  walimkuta mshitakiwa akiwa  ameondoka   ndipo   wananchi wa kijiji hicho  wakishirikiana na polisi  wa kituo  cha Kanoge  walipo weza kufanikiwa kumkamata mshitakiwa kabla ya kufika nyumbani kwake
Katika utetezi  wake mshitakiwa   aliomba  mahakama imwachie  huru  kutokana   na ushahidi ulio tolewa dhidi yake  kuwa ulikuwa  wa uongo 
Hakimu mkazi mfawidhi  Chiganga  alisema  mahamani hapo kuwa  katika kesi hiyo  ameridhika na  mwenendo mzima wa kesi kwa ushahidi  wa pande hizo mbili  za mashitaka   ambao  ulikuwa na mashahidi  wanne  na mshitakiwa aliye jitetea mwenyewe
Alisema kutokana  na ushahidi  huo mshitakiwa  amepatikana na hatia  ya kuvunja sheria  ya kifungu  namba  154  cha kanuni ya adhabu   cha marekebisho ya mwaka 2002
kutokana kosa  hilo  mahama imemuhukumu   mshitakiwa   Sindembali Msagi  kwenda jela  kutumikia  kifungo cha miaka 30 kwa kitendo chake  cha kumbaka  kikongwe huyo
Mahakama  wakati wa kuisikiliza kesi hiyo  illazimika  huhamia  nyumbani  kwa mama huyo  kusikilizia  kesi  hii kutokana  na kikongwe  huyo kutokuwa na hari nzuri ya kiafya   toka alipo fanyiwa kitendo hicho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa