Home » » POLISI WAKAMATA KATONI 16 ZA POMBE KALI KUTOKA NCHI JIRANI ZILIZOINGIZWA KINYEMELA

POLISI WAKAMATA KATONI 16 ZA POMBE KALI KUTOKA NCHI JIRANI ZILIZOINGIZWA KINYEMELA

Na Walter Mguluchuma
Mpanda jeshi  la Polisi  Wilaya   ya Mpanda  mkoa wa  Katavi  limekamata  katoni  16 za  pombe  kari  aina ya Vodka  zilizo ingizwa kutoka Nchi  jirani ya Burundi  bila kulipiwa ushuru
Kamanda wa polisi  wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari  alisema  pombe  hizo  ziiizo  kuwa zimetokea  Nchi  jirani ya Burundi zilikamatwa  hapo  Aprili  13 mwaka huu majira ya saa  12 jioni katika  maeneo  ya soko  la Bzogwe
Alimtaja aliye  kamatwa na pombe  hizo  kuwa ni  Hadija Hussein (40)  mkazi wa  Mkoa wa  kigoma  aliye  kamatwa  na pombe hizo muda mfupi  baada   ya  kuingia  mjini  Mpanda   akiwa  anatokea  Mkoani  Kigoma kwa  kutumia  basi  la kampuni  ya  Adventure
Alisema Hadija   alikamatwa kufuatia  taarifa  zilizo  lifikia jeshi  la polisi   kutoka  kwa raia  wema  kuwa  anajihusisha  na uwingizaji wa  pombe  karl  kutoka  Nchi  jirani   bila kulipia ushuru.
Kamanda Kidavashari  alieleza   baada  ya jeshi  la polisi  kupata  taarifa hizo   lilianza uchunguzi  wa kumfuatilia  mfanya biashara huyo wa kutokea Kigoma
Ndipo ilipo fikia   siku  hiyo  polisi   waliokuwa  wakiongozwa  na  Operation ofisa  wa jeshi  hilo  wa Mkoa  wa Katavi  Timithi   Nyika  walipo  fanikiwa  kumkamta  mtuhumiwa Hadija  akiwa na katoni  16 za pombe  kari aina ya Vodka
Kidavashari  alisema  mtuhumiwa  anatarajiwa  kufikishwa mahamani  mara  baada ya upelelezi  kuwa  umekamilika   mapema wiki lijalo
Jeshi  la polisi  Mkoa  wa Katavi limetowa  wito  kwa   wananchi   kutoa ushirikiano kwa  polisi  katika kuwafichua wafanya biashara wanao igiza bidhaa bila  kulipia ushuru  na kuisababishia Serikali kukosa  mapato
Baadhi ya  wafanya biashara  wamekuwa  wakikwepa kulipia  ushuru  wa bidhaa   zinazo toka katika Nchi za Burundi    na DRC kwa kupitia mwambao  mwa ziwa Tanganika

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa