Na Waler
Mguluchuma
Mpanda
Mahakama ya hakimu mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi imemuhukumu Yona Enerest (42) mkazi
wa Kijiji cha Majimoto Tarafa ya
Mpimbwe kifungo cha miaka sita jela kwa kosa
la wizi wa kuamiwa.
Hukumu hiyo ilitolewa hapo juzi na Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama
ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Tengwa baada ya kuridhika
na ushahidi ulio tolewa mahakamani hapo
Awali mwendesha mashitaka Inspekita msaidizi Ally
Mbwijo aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa Yona hapo April
mwaka jana alichukua jumla ya shilingi milioni
34 kwa Ismail Salehe mkazi wa Mkoa wa
Morogoro kwa lengo la kumnunulia mpunga
Alisema baada ya kuwa amepewa pesa hizo hakununua mpunga kama
walivyo kuwa wamekubaliana na kila alipo kuwa akiagizwa amtumie mpunga
wake alikuwa akimdanganya kuwa eneo ulipo mpunga kunatatizo la usafiri na
magari hayafiki huko
Mwendesha mashitaka Ally Mbwijo alieleza kuwa Isumail alipo
ona mpunga wake amechelewa kuupata aliamua kuufuatilia kwa mshitakiwa na
alipo ambiwa amkabidhi mpunga wake hata
hivyo mshitakiwa hakuweza kufanya hivyo
Hakimu mkazi Chiganga baada
ya kusikiliza uhahidi ulio tolewa mahakamani hapo alieleza kuwa
mshitakiwa amepatikana na hatia ya kujipatia pesa kwa
njia ya udanganyifu hinyo mshitakiwa Yona Ernest amehukumiwa
kifungo cha miaka sita jela na mali zake ziuzwe ili kulipia
deni la milioni 34
Wakati huo mahakama hiyo ya Hakimu mkazi imemuhukumu Lubeni Obedi (25) mkazi wa
kijiji cha Ilunde Wilaya ya
Mlele kifungo cha miaka mitano jela kwa
kosa la kuvunja na kuiba bidhaa mbalimbali za
dukani
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu mkazi mfawidhi wa
mahama ya wilaya ya Mpanda Chiganga Tengwa.
Mshitakiwa alidaiwa kiiba mafuta ya taa lita 40, viberiti vya
chuma 50, bunda 20 za sigara pamoja
na pesa tasilimu shilingi 15,000 mshitakiwa alidaiwa kutenda kosa
hilo hapo oktoba 15 mwaka jana
0 comments:
Post a Comment