Na Walter
Mguluchuma,
Mpanda.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mizengo Pinda kata ya Kibaoni Wilayani Mlele wamemshambulia kwa mawe
na matofali mkuu wa shule hiyo na mwalimu wa taaluma na kuharibu jengo la
utawala na nyumba za walimu hao baada
ya kuwatuhumu walimu hao kuwa ni washirikina.
Kaimu kamanda wa poli wa mkoa wa katavi Joseph Myovela alisema tukio
hilo limetokea hapo juzi majira ya saa 2:30 usiku
Alisema chanzo cha tukio hilo kilitokana na mwanafunzi mmoja hapo
juzi majira ya saa saba mchana kushikwa na ugonjwa wa mapepo uliomfanya aanguke
chini
Aalisema wakati akiwa ameshikwa na mapepo hayo aliwataja ALICO
Kamyoge (36) ambaye ni Mkuu wa shule hiyo ya sekondari ya Mizengo Pinda na
mwalimu wa taaluma Bonifasi Nsalamba (35) kuwa ndio wamemroga ugonjwa huu wa
mapepo
Myovela alisema ndipo ilipotimia muda huo wa saa mbili wanafunzi hao
walipojikusanya na kuandamana hadi kwenye jengo la utawala na kuanza
kulishambulia kwa mawe na matofali na kuweza kuvunja mlango na dirisha la jingo
hilo.
Alieleza baada ya kufanya uharibifu kwenye jengo la utawala
walielekea kwenye ofisi ya mwalimu wa taaluma ambapo waliharibu mtandao wa
mawasiliano kwenye Computer.
Wanafunzi hao ambao muda wote walikuwa na hasira walielekea nyumbani
kwa mkuu wa shule huku wakiwa na matofali na mawe walipofika na kumkosa mkuu wa
shule aliyekuwa amekwenda kwenye matembezi ya jioni walianza kushambulia nyumba
yake kwa mawe na tofali na kuharibu mlango na madirisha.
Kaimu kamanda Myovela alisema kisha kundi hilo lilielekea nyumbani
kwa mwalimu wao wa taaluma Bonifasi Nsalamba ambapo walimkuta akiwa anajiandaa
kuingia ndani ya nyumba yake akitokea matembezini.
Alieleza ndipo walipoanza kumshambulia kwa mawe katika sehemu
mbalimbali za mwili wake huku wakimzomea kuwa mchawi huyo mshirikina walizomea
hivyo.
Alisema katika shambulio hilo wanafunzi walimjeruhi mwalimu Bonifasi
na kumsababishia majeraha katika mwili wake na aliweza kutibiwa katika zahanati
ya kibaoni na kuruhusiwa na hari yake inaendelea vizuri.
Jeshi la polisi mkoa wa katai limetoa wito kwa wanafunzi wa shule
hiyo na shule nyingine za
mkoa huo waachane na kuamini imani za ushirikina na polisi inaendelea na
uchunguzi wa tukio hilo ili
kuwabaini waliohusika na waweze kuchukuliwa hatua.
0 comments:
Post a Comment