Na Walter Mguluchuma
Mpanda
Jeshi la polisi mkoa wa Katavi linamshikilia Albert Ades (25) mkazi wa Katandala Sumbawanga kwa tuhuma za kumuuwa Yassin Lupinda (22) kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali kufuatia marehemu kumwomba gazeti la kuvutia sigara
Kamanda wa poilisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri
kIdavashari alisema tukio
hilo lilitokea Aprili 12
majira ya saa 6 usiku katika
kambi ya uvuvi wa
samaki ya mtakuja Tarafa ya Mpimmbwe Wilayani Mlele Mkoa
wa katavi
Alisema siku hiyo ya tukio marehemu alikwenda kuomba gazeti la kuvutia sigara kwenye kambi jirani ya uvuvi aliyo kuwa akiishi mtuhumiwa
Kidavashari alieleza baada ya marehemu kufika kwa mtuhumiwa na na kueleza shida yake ya kuomba gazeti la kuvutia sigara mtuhumiwa alimweleza marehemu kuwa hayuko tayari kumpatia gazeti la kuvutia zigara
Marehemu Yassin aliendelea
kumsihi mtuhumiwa amsaidie kipande hata kidogo tuu cha gazeti kutokana na kiu kubwa aliyo kuwa aiisikia ya ya
kuvuta sigara
Hata hivyo mtuhumiwa aliona kama imekuwa kwake ni kero kwa marehemu kuendelea kumwomba kipande cha gazeti la kuvutia sigara
Kamanda Kidavashari alieleza ndipo marehemu alipo taka kuchukua gazeti kwa nguvu kitendo ambacho hakikumridhisha mtuhumiwa Albert
Ndipo ulipo tokea ugomvi na mtuhumiwa alipo mchoma marehemu kwa kitu chenye ncha kali sehemu ya kifua na kumfanya apige mayowe ya kuomba msaada
Majirani wa kambi za wavuvi walifika kwenye eneo hilo na walimkuta Yassin akiwa amegalagala chini huku akiwa amelala kwenye dimbwi la damu na walipo jaribu kumwinua waligundua ameisha kufa na wavuvi hao walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa muda huo huo
Kamanda Kidavashari alisema mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahamani kujibu shitaka la huhuma za mauwaji mara baada ya upelelezi utakapo kamilika
0 comments:
Post a Comment