Zaidi ya Shilingi Bilioni 4.5 zinatarajiwa kutumika
kwaajili ya mchakato wa awali wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Katavi ,
kinachotarajiwa kujengwa mjini Mpanda.
Akizungumzia ujenzi huo Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Mpanda Bw. Joseph Sebastian Mchina amesema kiasi hicho cha fedha kimepatikana ikiwa ni mkopo kutoka benki ya African Trade Insurance Agency (TIA).
Bw. Mchina amesema fedha hizo zitatumika kwaajili ya kulipa fidia ya eneo la ardhi lenye ukubwa wa hekari mia tano, ambazo zinatarajiwa kujengwa chuo hicho sanjari na gharama za andiko la mradi wa chuo hicho.
Mkurugezni huyo amesema chuo hicho kinatarajiwa kujengwa katika eneo la Kazima nje kidogo ya mji wa Mpanda ambapo katika matumizi ya fedha za awali pia mtaala wa chuo hicho utaandaliwa.
Amesema chuo hicho licha kujengwa mjini Mpanda kinatarajiwa kuwanufaisha wakazi wa mikoa jirani ya Rukwa na Kigoma ambapo katika hatua za ujenzi wa majengo yake jumla ya Shilingi Bilioni 650 zinatarajiwa kutumika ikiwa ni ruzuku kwa asilimia themanini na mkopo kutoka kwa Wafadhili kutoka nje ya nchi.
Akizungumzia ujenzi huo Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Mpanda Bw. Joseph Sebastian Mchina amesema kiasi hicho cha fedha kimepatikana ikiwa ni mkopo kutoka benki ya African Trade Insurance Agency (TIA).
Bw. Mchina amesema fedha hizo zitatumika kwaajili ya kulipa fidia ya eneo la ardhi lenye ukubwa wa hekari mia tano, ambazo zinatarajiwa kujengwa chuo hicho sanjari na gharama za andiko la mradi wa chuo hicho.
Mkurugezni huyo amesema chuo hicho kinatarajiwa kujengwa katika eneo la Kazima nje kidogo ya mji wa Mpanda ambapo katika matumizi ya fedha za awali pia mtaala wa chuo hicho utaandaliwa.
Amesema chuo hicho licha kujengwa mjini Mpanda kinatarajiwa kuwanufaisha wakazi wa mikoa jirani ya Rukwa na Kigoma ambapo katika hatua za ujenzi wa majengo yake jumla ya Shilingi Bilioni 650 zinatarajiwa kutumika ikiwa ni ruzuku kwa asilimia themanini na mkopo kutoka kwa Wafadhili kutoka nje ya nchi.
0 comments:
Post a Comment