Na Walter Mguluchuma
Mpanda
Mkazi wa Kijiji cha
Karema Wilaya Mpanda Mkoa wa Katavi
Jonas Ndegela ( 63) amefikishwa katika mahakama ya
Hakimu mkazi ya wilaya ya Mpanda kwa tuhuma
za kumbaka mtoto
wa dada yake mwenye umri wa mwaka
mmoja na nusu
Mwendesha mashika wa jeshi la
polisi wa jeshi la polisi Ally
Mwijo aliiambia mahakama mbele ya
hakimu mkazi mfawidhi wa mahama hiyo Chiganga
Tengwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Aprili 6
mwaka huu majira ya saa 5 asubuh
Mshitakiwa anadaiwa kuwa siku moja kabla
ya kufanya tukio hili alikuwa
ametokea kijiji cha Karema kwa
lengo la kumsalimia dada yake ambae ni
mama wa mtoto huyo aliye mbaka walio kuwa
wakiishi katika kijiji cha Mnyamasi Kata
ya Mpanda ndogo
Mwendesha mashitaka alieleza
kuwa siku hiyo baada
ya kuwa amefika kijijini kwa
dada
yake aliondoka na jirani ya mwenyeji
wake na
kwenda kwenye kilabu cha
pombe za kienyeji ambapo alikunywa
pombe na kuzidiwa na
kisha kulala kwenye kilabu hiyo ya
pombe za kienyeji
Mshitakiwa Jonas baada ya
kuamka alielekea nyumbani kwa dada
yake aliko kuwa amefikia ambapo
alipo fika hakumkuta dada
yake ila mlango wa
nyumba yake ulukuwa uko wazi
Hari hiyo ilimfanya mshitakiwa
aingie moja kwa moja ndani na ndipo alipo
ingia ndani alimwona mtoto huyo wa dada
yake akiwa amelala peke yake
Mshitakiwa alimwinua mtoto huyo
bila huruma alipo kuwa
amelala na kisha alivua nguo zake na kumweke juu
ya kifuu chake na
kisha alanza kumfanyia bila
huruma kitendo cha kumbaka huku mtoto huyo akipiga kelele
Mwendesha mashitaka aliendelea kuiambia
mahakama kaka wawili wa mtoto huyo walio
kuwa wameachiwa wamuangalie mdogo wao na mama yao aliye kuwa
amekwenda kisimani kuteka maji waliposikia mtoto
analia waliingia ndani aliko kuwa
amelala mtoto na walishitushwa kuona mjomba
wao akimfanyia unyama mdogo wao na
kuwafanya watoke nje haraka na kwenda
kuwaharifu majirani
Majirani walifika katika eneo
hilo na kumkuta mshitakiwa akiwa anajiandaa kuvaa
nguo zake alizo kuwa
amezivua huku mtoto huyo
akiwa akilia kutokana na maumivu makali
aliyo kuwa nayo
Mshitakiwa baada ya kuulizwa na
majirani kwani amemfanyia unyama mtoto
wa dada yake aliwaeleza kuwa ni kutokana
na pombe alizo kuwa amekunywa usiku kucha
Mshitakiwa alikana shitaka
na hakimu mkazi mfawidhi Chiganga aliharisha kesi
hiyo hadi hapo Aprili 25 kesi hiyo itakapo tajwa tena na na
mshitakiwa amepelekwa rumande
baada ya kunyimwa mdhamana
0 comments:
Post a Comment