Home » » AJALI YA BASI YAUWA WAWILI NA KUJERUHI .11

AJALI YA BASI YAUWA WAWILI NA KUJERUHI .11


   Na   Walter   Mguluchuma .
                   Katavi .
   Watu  wawili wamefariki  Dunia   hapo      hapo    na  wengine  11  kujeruhiwa na kulazwa   Hospitalini    baada  ya   basi  walilokuwa  wakisafiria   kutoka   Mpanda   kwenda   Tabora  kupinduka  baada ya kucha    njia .
Kamanda wa  Polisi  wa   Mkoa   wa  Katavi   Damas    Nyanda   aliwaambia   wandishi wa    Habari   jana  kuwa    ajari  hiyo  ilitokea  hapo   jana     majira  ya  saa  nane  mchana  huko     katika   eneo la   mlima   Kanono   Wilayani   Mlele   barabara   itokayo   Mpanda     kuelekea  Tabora  .
.
Aliwataja  marehemu   hao wawili  walikufa  hapo  hapo   kuwa  ni   Hilika   Maswalo   mwenye  umri wa  miezi mitatu  Mkazi wa  Kijiji  cha   Mwamapuli    Wilaya ya  Mlele   Mkoa  wa  Katavi   na  mtoto  mmoja   mwenye  mwenye  umri wa  mwaka  mmoja  ambae   amefahamika kwa   jina    moja   Baluhu   Mkazi wa  Tabora
 Ajari  hiyo  ilisababishwa   na    basi  hilo   kukatika   breki  wakati  likiwa   linashuka   kwenye   mlima   na  kasha  liliacha   njia   na   kupinduka na  kusababisha   vifo vya  watoto hao  wawili na  kujeruhi watu 11.

  Kamanda  wa  Polisi  Nyanda   alisema   ajari  hiyo   ililihusisha     basi    lenye  Namba  za  usajiri       T 258   DZD aina  ya   Scania   mali ya Boazi  Kemeu   Mkazi  wa   Mwanza la  Kampuni ya  BMK lililokuwa   likiendeshwa  na   John  Sadock   Mkazi wa  Mkoa  wa   Tabora ..
Bsi  hilo  la  Kampuni  ya   BMK   lilikuwa  likifanya   safari   kutoka   Mjini   Mpanda   Mkoani   Katavi  na   kuelekea    Mkoani   Tabora   kupitia  Wilayani   Mlele   Mkoani   hapa .
 Alisema  katika    ajari   hiyo  watu  11 walijeruhiwa  na  kulazwa  katika   Hospitali ya   Inyonga  huku  wanawake  wakiwa  saba  na  wanaume  wane   na   kasha    majeruhi  wanane  walipewa  rufaa  na  kuhamishiwa  katika   Hospitali ya  Wilaya  ya   Mpanda  ambapo  wamelazwa  na wanaendelea  kupatiwa   matibabu .
  Hari ya  majeruhi  waliolazwa   katika   Hospitali  ya  Manispaa ya  Mpanda   wanaendelea   vizuri   na  wale   watatu walilazwa  katika   Hospitali ya  Inyonga   wanaendelea  vizuri
Dreva  wa   basi hilo   anashikiwa  na  Polisi  na  anatarajiwa  kufikishwa  Mahakamani  mara  baada ya  uchunguzi wa   ajari  hiyo  utakapo  kuwa   umekamilika .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa