Home » » MWENYEKITI WA CCM KATAVI APIGA MARUFU WATU WALINZA KAMPENI YA UBUNGE 2020

MWENYEKITI WA CCM KATAVI APIGA MARUFU WATU WALINZA KAMPENI YA UBUNGE 2020



  Na  Walter Mguluchuma .
        Katavi .
  Mwenyekiti wa  Chama  cha  Mapinduzi  CCM    wa  Mkoa  wa   Katavi   Mselemu   Abdala    amewagiza    Makatibu  wa   CCM  wa   Wilaya  zote za  Mkoa  huu   kuwachukulia   harua  mara   moja   wanachama  wa    Chama  hicho  ambao  wameanza  kufanya  kampeni kwa   ajiri ya  kugombea  Ubunge na  Udiwani    kwa     ajiri   ya  uchaguzi  mkuu   ujao  wa mwaka  2020.
Agizo  hilo   alilitowa  hapo  juzi   wakati   alipokuwa  akiwahutubia   wananchi  wa  Tarafa  ya  Inyonga   Wilayani   Mlele   kwenye   uwanja  wa   shule   ya  Msingi   Inyonga   Jimbo  la  Katavi .
  Alisema  wapo   baadhi ya   wanachama wa   CCM ambao  wameanza  kufanya  kampeni za  kugombea   Ubunge  wa  mwaka   2020   wakati  ni   kinyume  na  utaratibu  wa   Chama  hicho .
Namnukuu  wacheni  viongozi  walioko  madarakani   waendelee  kufanya  kazi  kwenye   majimbo  yao  kwani  watu  kuanza  kufanya  kampeni  kwenye   majimbo  yenye   Wabunge    mnawachanganya  walioko   madarakani    sasa .
 Aligiza  kuwa   Makatibu  wote  wa  Wilaya  wa   chama  hicho  waakikishe   kuwa  wanawadhibiti watu  wote   ambao  wameanza  kufanya  kampeni   kwenye   baadhi ya  majimbo ya   uchaguzi   katika   Mkoa wa  Katavi .
Mwenyekiti  huyo wa  Mkoa  wa  Katavi   Mselemu  Abdala   alieleza  kitendo   cha  watu  kuanza  kufanya   kampeni  wakati  huo   kutawafanya   viongozi wa    majimbo   hayo  kushindwa  kufanya  kazi  zao   vizuri .
Alisema  wakati huo   sio  kipindi  cha   kufanya   siasa   bali ni  wakati wa  kufanya  kazi    anae   taka   siasa   asiburi  hadi  mwaka     2020   ndio  muda wa  kufanya   siasa .
Kauli  hiyo ya  Mwenyekiti wa    CCM  alitowa   agizo  hilo   baada ya  kuwepo   kwa  taarifa  za  kuwa    kuna   mwanachama  mmoja   ameanza  kufanya   kampeni  katika   jimbo  la  Katavi  linaloongozwa  na   Naibu  Waziri  wa   Maji na  Umwagiliaji     Eng   Izack  Kamwelwe  kwa  ajiri ya  uchaguzi wa  mwaka   2020 .
Kwa  upande  wake  Mkuu wa  Wilaya  ya   Mlele    Lechor  Kasanda   alieleza  kuwa  Wilaya  hiyo  imeisha   anza  mikakati ya  ujenzi wa  vyumba  vya   madarasa  ,  nyumba za  kuishi  walimu  na  ujenzi wa vyoo  bora vya  kisasa .
Alisema   anatowa   wito kwa   Wananchi  kuunga  mkono  jitihada  hizo  za   Serikali ya   Wilaya  hiyo kwa  wananchi kuchangia  michango  mbalimbali  ilikuweza  kufanikisha  ujenzi huo .
Dc   huyo  alieleza  kuwa   Serikali ya  Wilaya  hiyo imewaagiza    wananchi  wa  Wilaya  hiyo  kuhakikisha   kwa  kipindi cha  miezi  mitatu   kuwa   kila     mmoja   we  amejenga  choo  bora  na  cha  kisasa  kwenye  nyumba  yake  na  baada  ya   kupita  kipindi  hicho  timu  ya  wataalamu wa   afya  watapita  kwa  ajiri ya  ukaguzi  na    watakao kuwa  wamebainika   kushindwa  kutekeleza   agizo la  kuwa  na  choo   bora    na  cha  kisasa  watachuliwa   hatua  alisema    Dc  Kasanda

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa