Home » » DC MLELE ATOWA AGIZO KWA WATUMISHI .

DC MLELE ATOWA AGIZO KWA WATUMISHI .


Na  Walter   Mguluchuma.
      Mkuu wa  Wilaya ya Mlele  Mkoa wa  Katavi   Rachael  Kassanda  ametowa  agizo kwa  Watumishi wa Wilaya  hiyo  kutofanya kazi kwa mazowea  hari  ambayo inasababisha  Wananchi  kutopata  huduma zao  kikamilifu  na kwa wakati.
 Mkuu  huyo wa  Wilaya  alitowa  agizo  hilo  hapo jana  wakati  alipokuwa  akizungumza  na  watumishi wa  ofisi ya   Mkuu wa  Wilaya  hiyo  na  watumishi wa  Halmashauri ya  Wilaya ya  Mlele  katika   kikao  cha utambulisho wake kilichofanyika  katika  ukumbi wa  shule ya  Sekondari  Inyonga.
 Alisema  ili  mtumishi  aweze kutekeleza  majukumu  ya  kuwahudumia  wananchi  kwa  wakati muafaka  ni  lazima  kuwe  na   mpango kazi  utakao  mwongoza  katika  kutekeleza    shughuli  za  kiutumishi  na  ambao   utakuwa   dira ya  kuhakikisha   sera ya  hapa  kazi tu inazingatiwa.
  Alifafanua  kuwa  watumishi  wengi  wakuwa  hawatekelezi  majukumu  yao ya  kazi  ipasavyo  kwa  ajiri ya  tabia ya kufanya  kazi kwa  mazoea  hivyo  watumishi  wanaofana  kazi kwa  mazoea  waache  mara  moja .
  Sambamba   na  hilo   Mkuu wa  Wilaya   Kassanda   aliwataka  watumishi  kusafirisha   nyaraka  za   Serikali  kwa  njia   sahihi   na   inayotambulika   Kiserikali   ili  kuhakikisha  usalama  wa  nyaraka  husika  na  utunzaji  wa  siri   za  Serikali  kwa  mujibu  wa  kanuni  na  taratibu  za  kiutumishi .
  Alisema  kumekuwa  na  mazoea  ya  watumishi  wa  Serikali  kutumiana   nyaraka   za  Serikali  kwa  njia   ambazo  sio  halali  ikiwa  ni   pamoja  na  barua   pepe  ambazo   hazina  umiliki  wa  Serikali  ambazo ni  yahoo, Gmail  Hotmail  Rocketmail,na  Whatsaap.
 Hivyo  mtumishi yoyote wa  Serikali  ambae  atasafirisha  nyaraka za  Serikali  katika   Wilaya  yake ya  Mlele   kwa  njia  isiyo  sahihi  atahakikisha  anachukuliwa  hatua  kali za  kinidhamu  za kiutumishi .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa