Home » » WAFUGAJI WAILALAMIKIA ERIKARI MKOANI KATAVI KWA KUSHINDWA KUTENGA MAENEO YA WAFUGAJI.

WAFUGAJI WAILALAMIKIA ERIKARI MKOANI KATAVI KWA KUSHINDWA KUTENGA MAENEO YA WAFUGAJI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



 Baadhi ya wafugaji wa Kijiji  cha  Katambike  Kata ya ugala Wilata ya Mlele  wakitowa  malalamiko yao  ya  kuwashutumu watumishi wa Maliasili wanavyo wanyanyaa wafugaji  malalamiko  hayo waliyatowa  hapo  jana  kwenye kikao kilichofanyika  katika  ukumbi wa  Maji  Mjini hapa  kwa   Katibu Mkuu wa chama cha  wa wafugaji  Tanzania  Magembe  Nkonosenema ambae  hayupo  pichani 
Makamu  Mwenyekiti wa  Halmashauri ya  Wilaya ya  Mpanda  Thiodela  Kisesa akiwahutubia  wafugaji wa   Mkoa wa  Katavi katika  kikao  kilichofanyika  jana  katika  ukumbi wa  idara ya  maji ambapo  aliwataka watumishi  wa idara ya  maliasili kufanya  kazi kwa  kufuata  utaratibu na heria  na wafugaji   waache  kuishi maeneo ambayo  hayasitahili waishi .
  Picha  Na  Walter  Mguluchuma  Katavi yetu Blog

 

N a  Walter  Mguluchuma
               Katavi
Chama  cha   Wafugaji   Mkoa  wa   Katavi  CCWT wameilalamikia      Serikali ya  Mkoa wa  Katavi  kwa kushindwa   hadi sasa  kutenga maeneo  ya  kuchungia  mifugo  kama  ambavyo  alivyoagiza  Makamu wa  Rais Samia Suluu  Hassani    kufanya hivyo kwa Mikoa yote hapa  Nchini.
Hayo   yalisemwa  hapo  jana  na   Mwenyekiti wa  chama  cha  wafugaji   CCWT   Mkoa  wa  Katavi     Mussa Kabushi   mbele ya  Katibu Mkuu wa    Taifa wa  Chama  cha  Wafugaji  Tanzania  Magembe   Nkonosenema  wakati  kikao   cha wafugaji wa Mkoa wa  Katavi  kilichofanyika  jana   katika  ukumbi wa  Idara ya  Maji  na kuhudhuliwa  na  viongozi wa  Halmahauri ya  Wilaya  ya  Mpanda .
 Aliema  Serikali  imeisha  towa  agizo  la kutengwa  kwa  maeneo kwa  ajiri ya  kulishia  mifugo  lakini   mpaka  sasa    wafugaji wa  Mkoa  wa  Katavi   hawaja  tengewa  maeneo  hayo  na  matokeo  yake wafugaji  wamekuwa wakikamatiwa  mifugo yao  na kutozwa  faini  tena  bila  kupewa  risiti  za  malipo wanayotozwa.
 Hivyo   chama   cha  wafugaji  kinaiomba   Serikali   iharakishe  kutenga  maeneo ya  malisho  kama walivyo  agizwa  na  Makamu wa  Rais   Samia  Suluu  Hassan ilikuepusha   migogoro  kati  ya  wakulima,  na  wafugaji na   Serikali .
Kabushi  alieleza   chama  cha  wafugaji  kimebaini  endapo    yatatengwa   maeneo ya  malisho,  na mifugo  kukaa   sehemu  moja   katika   mashamba   rasmi wataondoa   kero  za   uharibifu  wa  mazingira  na mwingiliano   na  sekta   zingine  kwani kwa  takwimu walizo  nazo   mpaka  sasa  Mkoa  una   Ng-ombe  695,433.
Chama  cha  wafugaji   kimekubaliana  na  wafugaji  wote wa  Mkoa huu  kwa   pamoja  maeneo yote  yatakayotengwa  kwa  ajili ya  malisho  watakuwa  wanachangia  na  kulipia  kwa  kila   kichwa   Ng-mbe  Tsh 5,000 ambapo     Tsh  2,000  zitakwenda  kwenye   kwenye  Halmashauri  husika  na    Tsh  3,000 zitakwenda  kwenye  mfuko wa   chama  cha wafugaji   kwa  ajiri ya  kuendeleza  na kulitunza   eneo  watakalo tengewa wafugaji .
  Nae  Katibu wa  CCWT   Mkoa  wa  Katavi  Mahela   Mayanda   alisema  wafugaji  wamekuwa  wakikamatwa  na   Askari wa  Hifadhi   pamoja   na  maliasili  na  wamekuwa  wakiteswa   vikali   ikiwa  pamoja  na kutozwa   faini za juu zinazofikia  milioni  15  hadi  milioni  20 na kutokuwa  linganifu  na  idadi  ya  Ngmbe  wanazizikamata  na  kunyimwa   stakabadhi ya  faini  hizo .
 Alizungumza  kwa  masikitiko   makubwa   alisema   zaidi ya  Ng-0mbe 5,840 wameuwawa  kwa kupigwa  risasi katika kipini cha mwaka 2013 hadi 2015   kutokana  na  kuwa  ndani  ya  eneo la    Rukwa   Lwafi  lililotengwa   kama  eneo la  pori  la  akiba .
Katibu  mkuu wa   chama  cha  Wafufaji  Tanzania   Magembe    Nkonosenema   zipo  changamoto   nyingi  sana   zinazo  wakabili  wafugaji wa  Mkoa  wa   Katavi .
  Alisema   chama  cha  wafugaji   hakitaki wala  hakipendi  kuwa  na  malumbano  na   Serikali   bali   wao  wanachohitaji ni   Serikali  kutenga  maeneo ya  wafugaji kwani   shughuli ya  ufugaji   sekta  rasmi na  ndio  maana  Rais  alimteuwa  waziri   anae   shughulikia Wizara ya   mifugo.
Sanjari  na  hayo    Nkonosenema alisema   kumekuwepo na   tabia  ya uanzihwaji  wa  mapori ya  akiba WMA    nanayoanzishwa   kiujajanja   na wamekuwa wakipewa  maeneo  hayo  Wazungu   badala  ya wazawa.
Makamu   mwenyekiti  wa  Halmashauri ya  Wilaya  ya  Mpanda  Thiodela  Kisesa   aliwataka  wafugaji  wafuate   sheria  na  waishi   kwenye  maeneo  yaliotengwa kuishi .
 Alisema wapo  baadhi ya  viongozi wa siasa wamekuwa  wamekuwa wakiwalazimisha  wafugaji kuishi  kwenye  maeneo  yasiyo  sitahili  kuishi wafugaji wa  mifugo .
Alieleza  kuwa   Halmashauri ya  Wilaya  ya   mpanda  ipo  kwenye  utaratibu wa kupanga  matumizi ya   ardhi   katika  maeneo  yote  ya  Halmashauri  ya   Wilaya  ya  Mpanda   hari  itakayosaidia kupumguza  migogoro ya  wakulima  na  wafugaji

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa