Home » » MKUU WA WILAYA ACHANGISHA MADAWATI 200 YENYE THAMANI YA TSH MIL 13

MKUU WA WILAYA ACHANGISHA MADAWATI 200 YENYE THAMANI YA TSH MIL 13

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  Paza Mwamlima   amechangisha zaidi ya madawati 200   yenye thamani ya zaidi ya  shilingi milioni 13 katika kikao alichokifanya na wadau wa Elimu wa Manispaa ya  Mji wa Mpanda.
Kikao hicho cha aliwaeleza wadau wa elimu kwenye kikao hicho kuwa Wilaya ya Mpanda inakabiliwa na upungufu wa madawati zaidi ya 13,000 katika shule za msingi na  sekondari .
Aliwaeleza Manispaa ya  Mpanda inakabiliwa na upungufu wa dawati  zaidi ya 5,400na  Halimshauri ya Wilaya ya Mpanda  zaidi ya dawati 7,700 huku mpaka sasa zaidi ya dawati  2600 zimeisha tengenezwa na kukamilika.
 Alisema wilaya ya Mpanda imejiwekea mikakati  mbalimbali ya kuhakikisha inakamilisha  madati hayo ifikapo mwezi june mwaka huu.
Alizitaja baadhi ya mikakati hiyo ni  kila mkuu wa idara kuchangia kiasi cha shilingi laki moja na kila mbao na magogo yanayokamatwa  hutaifishwa na kutengenezwa matofaii pia wameruhusu uvujanaji wa miti ya mbao kwenye misitu ya Kijiji cha kufuata sheria za mistu.
Mkuu huyo wa Wilaya  baada ya kutowa maelezo hayo aliwaomba wadau hao wa Elimu waweze kuchangia fedha au  dawati pamoja na vifaa vya kutengenezea madawati .
 Wadau hao wa elimu waliitikia wito huo ambapo walichangia  jumla ya dawati 224 zenye  thamani ya Tsh13,440,000 na  fedha kiasi cha  shilingi  milioni  5,650,000.
Wilaya ya Mpanda  imekuwa na kasi kubwa ya ongezeko la wanafunzi waliojiandikisha darasa la kwanza la  awali ambapo  darasa moja baadhi ya shule wanafunzi wamejiandikisha 800.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa