Home » » CWT MPANDA YAIOMBA SERIKALI KULIPA MAFAO YA WAALIMU WASITAAFU KWA WAKATI

CWT MPANDA YAIOMBA SERIKALI KULIPA MAFAO YA WAALIMU WASITAAFU KWA WAKATI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


   Na  Walter  Mguluchuma
   Katavi
Chama  cha  waalimu  CWT   Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  kimeiomba  Serikali  kuhakikisha
inawalipa   Waalimu wanao sitaafu malipo yao ya kinua mgongo pindi wanapo sitaarifu kuliko ilivyo sasa ambapo baadhi ya wasitaafu wamekuwa wakifariki Dunia huku wakiwa hawajalipwa mafao yao ya kinua mgongo
Hayo lisemwa  hapo jana  na  katibu wa  chama  cha waalimu  Wilaya  ya  Mpanda   Wilson  Masolwa   mbele ya  mwakilishi  wa  Katibu mkuu wa  CWT  Taifa   Costantine Marcely  kwenye risala ya  chama  hicho aliyoisoma wakati wa  sherehe  za  kuwaaga waalimu waliositaafu  kutoka  katika  Halmashauri  za  Wilaya  ya  Mpanda  na  Halmashauri ya  Nsimbo  zilizofanyika  katika  ukumbi wa Kanisa  Katoliki Jimbo la  Mpana  mjini  hapa.
Masolwa  alisema  waalimu  wanaositaafu  wamekuwa  wakikabiliwa  na   changamoto  ya kutolipwa  mafao yao  ya kinua  mgongo  kwa wakati  pindi wanapokuwa wamesitaafu  hali  ambayo imekuwa  ikipelekea  baadhi ya waalimu wasitaafu kufariki  Dunia  kabla hawaja  lipwa  mafao yao .
 Alieleza  kutokana na waalimu wanao kuwa wamesitaafu na kushindwa kulipwa kwa wakati  CWT  Wilaya ya  Mpanda inaiomba  Serikari kuhakikisha inawalipa walimu wote wanaokuwa wamestaafu mafao yao kwa wakati .
Risala  hiyo ilieleza pia  kuwa waalimu  wanaokuwa wamestaafu wamekuwa wakikabiliwa pia  na  changamoto ya kutolipwa  fedha  za  nauri ya kuwarudisha makwao hari  ambayo imekuwa ikisababisha wasitaafu waishi maishi ya shida wakati wakiwa wanasubiria   fedha za kuwarudisha kwao.
Changamoto nyingine nyinine  waliitaja kuwa ni  wasitaafu kucheleweshewa kupewa vitambulishi vya  Bima ya  afya  pindi wanapokuwa wamesitaafu wamekuwa haepewi vitambulisho hivyo kwa wakati .
Katika  sherehe  hizo za kuwapongeza  waalimu waliositaafu kumi na moja  chama  hicho kiliwapatia waliamu waastaafu kila   moja   bati  ishirini  ambapo kila  msitaafu mmoja  alipewa  bati  zenye  thamani ya  Ts  340,000 kutoka  kwa  CWT  Wilaya  ya  Mpanda.
Kwa upande wake mwakilishi wa  Katibu  mkuu Taifa wa CWT  ambae pia ni katibu wa  Chama  cha waalimu Mkoa  wa  Katavi Costantine  Marcely  alisema  chama  cha waalimu    kitaendelea  kupigania  masilahi ya waalimu .
 Alisema kila  mwaka jumla ya waalimu  7500 husitaafu   hapa  nchini na alitoa  mfano kuwa  ukiona  dume  la  nyani limezeeka ujuwe limekwepa  mishale  mingi hivyo kwa wataafu hao paka kufikia hatua  hiyo wamepitia misuko suko mingi.
Marcely  alieza   CWT  imeisha  weka utaratibu kuanzia julai mwaka  jana wa   kuwazawadia bati 20 wanachama wake wote wan chi nzima wanaokuwa wanastaafu  ikiwa ni sehemu ya kuheshimu michango yao walitowa  ndani ya  chama hicho na  mfuko utakapo kuwa mkubwa wataangalia namna ya kuboresha zawadi kwa wastaafu .
Nae  mstaafu  mwalimu  Venansi Nkanga  alisema wakati walipokuwa wanaanza kazi mazingira ya utumishi yalikuwa ni magumu kuliko ilivyo sasa kwani wakati huo hari ya miundo mbinu ya barabara ilikuwa ni mibovu .
 Alisema kazi ya ualimu ni nzuri  ni  nzuri  pale unapoipenda  hivyo aliwaasa waalimu abao bado wanaendelea kufundisha waipende kazi ya ualimu.
Kwaupande wake mstaafu mwalimu Sebastiani  Mdula  aliwataka waalimu wanaobaki  wafanya kazi kwa bidii na nidhamu  na  kama  hawata  fanya  hivyo  wataona  kazi ya ualimu  ni    ngumu.
Mwenyekiti wa  chama  cha  waalimu  Mkoa  wa  Katavi   john  Mshota  aliwataka  waalimu  kufanya  kazi kwa kuzingatia  maadili na kuacha  tabia  ya kutongoza wanafunzi wao wanaowafundisha kwani ni kinyume cha maadili ya utumishi .
Na  chama  hicho  hakitakuwa  tayari kumtetea  mwanachama wake ambae  anavunja  maadili ya utumishi kwa makusudi alisema  mwenyekiti huyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa