Home » » DC ATOA AGIZO LA JENGO LA KULAZA WAGONJWA LIFUNGULIWE

DC ATOA AGIZO LA JENGO LA KULAZA WAGONJWA LIFUNGULIWE



Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter  Mguluchuma
  Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima  ametowa agizo kwa uongozi wa Hospiali ya Wilaya ya Mpanda  kuhakikisha inalifungua  jingo la wodi  la kulaza wagonjwa  ambalo limeisha kamilika   huku likiwa halitumiki  wakati wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo wanalala wawiliwawili.
Mwamlimu alitowa agizo hilo hapo jana wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo alipokuwa akizungumza na watumishi hao kwenye hospitali hiyo wakati wa ziara yake aliyoifanya ya kuangalia  changamoto mbalimbali zinazo ikabili hospitali hiyo.
Alisema nijambo la kshangaza kuona wagonjwa katika hospitali hiyo wanalala wawili wawili wakati kuna jingo jipya  ambalo limekaa bila kuwa linafanya kazi  huku likiwa linaanza kuchakaa.
Aliwatowa agizo  ndani ya siku saba kuanzia jana kwa jingo hilo kuwa limeanza kutumika kwani yeye hayuko tayari kuona wagonjwa wanalala wawili wawili katika hospitali hiyo wakati kuna jingo la wodi lipo wazi alifanyi kazi.
Mwamlima pia  aliwataka watumishi wa afya kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa  na kwauadilifu mkubwa  katika majukumu yao na wafanye kazi kwa uzalendo zaidi .
Alisema wapo  baadhi ya watumishi wa afya wamekuwa wakiwatorea lugha mbaya wagonjwa wakati wakiwa wanawaudumia  hivyo hata sita kumchukulia mtumishi yoyote ambaye atakae bainika kufanya hivyo.
Dc  huyo alizungumzia kuwepo kwa baadhi ya watumishi ambao sio waaminifu ambao wamekuwa na tabia ya  kuwauzia damu wagonjwa wakati damu inatolewa bure.
  Alisema  madaktari na wauguzi wanapaswa kujitambua kuwa wao ni watu muhimu kwa kuwa shughuli  zao zinahusu uhai wa  binadamu .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa