Home » » DC MPANDA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUWAELISHA WATU WASIKATE MITI OVYO

DC MPANDA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUWAELISHA WATU WASIKATE MITI OVYO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Walter Mguluchuma
 Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza  Mwamlima amewataka waandishi wa Habari kuwaelimisha  jamii kuacha kukata miti ovyo ili kuweza kusaidia kuzuia  uharibifu wa mazingira .
Mwamlima alitowa wito huo hapo  jana wakati alipokuwa akizungumza na  wafanya biashara wenye viwanda vidogo vya  kuchana mbao katika eneo la Pasifiki   Mtaa wa Majengo B Manispaa ya Mpanda .
 Alisema  hari ya ukataji ovyo wa miti na  uharibifu wa mazingira umekuwa ni mkubwa sana katika Mkoa wa Katavi na  hari hiyo ikiendelea hivyo upo uwezekana mkubwa wa kutokea jangwa  katika Mkoa huo ambao unasifika kuwa na uoto  mzuri  wa mistu kuliko mikoa mingine hapa Nchini .
 Alisema ilikukabiliana na  hari hiyo  waandishi wa habari  wanao wajibu mkubwa wa kuielimisha  jamii kuacha  tabia ya  kukata  miti ovyo  ilikuinusuru Wilaya hiyo na Mkoa wa Katavi  kuwa najangwa.
Mwamlima alieleza waandishi wa habari wanayo nafasi kubwa ya  kuelimisha watu  umuhimu wa kutunza mazingira  kutokana na nafasi yao walionayo kwenye jamii.
 Wapo baadhi ya watu  wamekuwa wakifanya uharibifu wa mazingira kwa  kwa kukata miti ovyo ,kuchoma mapori na kufyeka ovyo mistu  kutokana na kutokuwa na  uwelewa  wa kujua umuhimu wa kutunza mazingira.
 Hivyo vyombo vya habari  vione  na vitambue  vinaumuhimu  sana wa kuwaelimisha watu  kutunza mazingira  yanayowazunguka  kwenye vijiji vyao na kwenye mitaa yao
Alieleza swala la  kuelisha jamii kutunza mazingira  waandishi wa habari wasilione kuwa ni la serikali peke yao bali walione swala hilo ni jukumu lao.
 Mkuu huyo wa Wilaya alisema hari ya uharibifu wa mazingira umekuwa ukiongezeka kwa kasi kubwa katika Wilaya hiyo na mkoa kwa ujumla kutokana na watu  kutoona umuhimu wa  kutunza mazingira kitu ambacho ni hatari kwa Mkoa huu  na Nchi pia.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa