Home » » SERIKAKI WILAYANI MPANDA WASITISHA UTOAJI WA VIBARI VYA UVUNAJI WA MBAO ZA MITI YA ASILI

SERIKAKI WILAYANI MPANDA WASITISHA UTOAJI WA VIBARI VYA UVUNAJI WA MBAO ZA MITI YA ASILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Walter Mguluchuma
   Katavi
Serikali Wilayani Mpanda Mkoani Katavi  imesitisha utoaji wa  vibali vya uvunaji wa  miti ya asili  inayovunwa kwa ajiri ya  mbao na magogo  kutokana na kuwepo kwa  uharibu  mkubwa wa  mistu  katika Wilaya ya Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla.
Agizo hilo lilitolewa hapo jana na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima  wakati alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara  wenye viwanda  vidogo vya  kuchana mbao na kutengeneza  vitanda na mirango ya mbao pamoja na samani za ofisi na nyumba  kwenye  eneo la Pasifiki Mtaa wa Majengo Mjini hapa.
 Alisema kuanzia sasa  Serikali ya Wilaya ya Mpanda imesitisha utoaji wa vibali vipya  vinavyo waruhusu watu wavune miti ya mbao ya asili kutokana na uharibifu  mkubwa ambao umefanywa  wa uharibifu wa mistu  katika Mkoa wa Katavi uliosababishwa na uvunaji holela wa  miti ya mbao.
Mwamlima  alieleza  kuwa  kutokana na uharibifu mkubwa wa  mistu unaoendelea  kufanywa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi  Serikali ya Wilaya hiyo imeamua kusitisha utoaji wa vibali vya uvunaji wa  miti   ya mbao  na magogo  na kwa wale ambao walipatiwa vibari  hawata pewa tena vibali vingine  mara baada ya vibali vyao vitakapo kuwa vimekwisha.
Alisema  atakae kamatwa na mbao haramu  afungwe na kupewa faini kubwa  ili iwefundisho  kwa watu wengine wanao  fanya biashara haramu ya uvunaji wa miti ya mbao.
Atakae taka kibali cha kuvuna mbao  atapewa kibali cha kuvuna miti ya kupanda na  sio kuvuna miti ya asili kama ilivyo sasa hivyo wahakikishe  wanapanda miti kwa ajiri ya kuvuna mbao .
Mkuu huyo wa Wilaya  pia ameagiza  mbao zote ambazo zilikamatwa  zikiwa  vimevunwa na  wavunaji haramu   zisipigwe mnada  na zitumike kutengeneza  madawati ya wafunzi .
Afisa Mistu Wilaya ya Mpanda Lucas Nyambala  aliwataka wanye viwanda vidogo hivyo kuacha tabia ya kununua mbao kwa watu wasio na vibali  badala yake wanunue kwa  watu wenye vibali vya kuvuna mbao.
Mwenyekiti wa wenyeviwanda  vidogo vya Pasifiki Sailoni Mhagama  alieleza kuwa waharibifu wakubwa  wa mistu  ni wenye leseni kubwa na sio wenye leseni ndogo  hivyo Serikali ya Wilaya ya Mpanda ingewapiga marufuku Raia wa Nchi ya China wanaofanya shughuli ya uvunaji  wa magogo  katika Mkoa wa Katavi  kutokana na uharibifu mkubwa wanofanya wa kuharibu mistu .
Aliomba  mbao zinazovunwa katika Mkoa wa Katavi  zisiwe zinasafirishwa  kutoka nje ya Mkoa huu ili watu wa Mkoa huu waweze kunufaika  kwani mbao moja ya mti wa mninga inauzwa kati ya shilingi elfu kumi na nne na kumi na sita.
Nae Moshi Dede alieleza kuwa  agizo hilo la kusitisha  utoaji vibali  vya   uvunaji  wa miti ya mbao ya asili utawaathili kwani miti ya kupandwa hutowa mbao zenye rangi nyeupe ambayo haipendwi na watu waliowengi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa