Home » » WAWILI WAFA KWA RADI NA WATATU KUJERUHIWA

WAWILI WAFA KWA RADI NA WATATU KUJERUHIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Watu wawili  Lupimwa  Julias(30)  na Remi  Madirisha (32) wakazi wa Kijiji cha Ilebula Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Mpanda wamekufa hapo hapo  baada ya kupigwa na radi na wengine watatu kujeruhiwa wakati wakiwa shambani.
 Tukio la  vifo vya watu hao wawili lilitokea hapo juzi  majira ya saa  kumi na nusu jioni Kijijini hapo wakati watu hao wakiwa shambani kwao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari  aliwaambia jana waandishi wa Habari kuwa watu watatu waliojeruhiwa na Radi hiyo kuwa ni  Tatu Jerald ,Stela John na  Filiberti Paskali  wote wakazi wa Kijiji cha Ilebula Wilayani hapa.
Alisema kabla ya  tukio hilo marehemu hao wawili  na majeruhi  walikuwa shambani kwao wakiwa wanalima  shamba lao  lililiopo kwenye Kijiji hicho.
Wakati wakiwa wanaendelea kulima  mvua ilianza  kunyesha  ambapo wote waliamua  kwenda  kujikinga  chini ya mti  uliokuwa  kwenye shamba lao.
Kamanda Kidavashari  alieleza   ndipo  watu hao Radi ilipowapiga  na kupelekea  vifo vya watu wawili na kujeruhi  watatu.
 Alisema  baada ya tukio  majeruhi wote watatu  walipelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  na wanaendelea na matibabu  katika wodi namba  moja waliko lazwa huku hari zao zikiwa zinaendelea vizuri .
Na miili ya marehemu wamekabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya maandalizi ya mazishi yatakayo fanyika  kesho  katika makabuli ya Kijiji cha Ilebula.
Kamanda Kidavashari  amewatahadharisha  wananchi wa Mkoa wa Katavi  kuwa makini  katika kipindi hiki cha masika  pindi mvua zinaponyesha  kujihifadhi  maeneo yaliosalama

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa