Home » » MANISPAA YA MPANDA KUTENGENEZA BARABARA ZA RAMI ZAIDI YA KILOMETA SABA

MANISPAA YA MPANDA KUTENGENEZA BARABARA ZA RAMI ZAIDI YA KILOMETA SABA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
 Manispaa ya  Mji wa Mpanda Mkoani Katavi  inatarajia kuanza ujenzi wa Barabara   zake  karika  Manispaa hiyo  zenye urefu wa kilimeta7.7 kwa  kiwango cha Rami zitakazo  gharimu   kiasi cha  shilingi milioni 350.
 Haya yalisemwa hapo jana  na Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Selemani Lukanga  kwenye  kikao cha pili cha Baraza la Madiwani  wa Manispaa hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda katika Mtaa wa Ilembo Mjini hapa.
Awali Diwani wa Kata ya Makanyagio Haidari Sumry alitaka kujua  Manispaa hiyo inampango gani  wa kutengeneza barabara zake kwa kiwango cha rami na zitagharimu  kiasi gani cha fedha.
 Kufuatia swali hilo la Diwani wa Makanyagio  Mkurugenzi huyo alilieleza Baraza la Madiwani kuwa  katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha wa 2015 na 2016 wanatarajia kujenga Barabara  zenye  urefu wa kilometa 7.7  zitakazogharimi kiasi cha shilingi milioni 350.
Lukanga aliiambia Baraza hilo barabara zitakazotengenezwa  ni katika Mitaa ya Kashauli  ,Kawajense  Nsemlwa  na  Mtaa wa Madukani .
Pia  aliliambia Baraza la Madiwani kuwa Manispaa hiyo imepata kibali  cha kajiri watumishi  195 wa kada mbalimbali  ambao watasaidia kupunguza tatizo  la upungufu wa Watumishi.
Watumishi ambao wanatarajiwa  kuajiriwa ni  watumishi wa afya, Waalimu. watendaji wa mitaa, maafisa ugavi ,wahasibu na wakaguzi wa ndani .
Meya wa Manispaa   Wiliy Mbogo  kwa upande wake alieleza  kuwa Manispaa imepanga  kuhakikisha maeneo ya Manispaa yanapimwa ili kuufanya  Mji kuwa katika mpango mzuri na kuwafanya watu wasijenge kiholela
Pia wanatarajia kuweka alama  kwenye maeneo ambayo watu wamejenga kiholela ili waweze kujitambua kabla ya hatua ya kuwabolea  na kuwaondoa kwenye maeneo hayo haija anza.
Afisa  usitawi  wa jamii wa timu  salama ya damu Redguarda Mayolwa alieleza jumla ya watu 430 wamejitolea kuchangia damu  salama kwa kipindi cha mwaka jana  ambapo ziliweza kupatikana uniti 430 za damu salama.
Madiwani wa Baraza hilo waliomba hatua za haraka zichukuliwe za Manispaa hiyo kukabidhiwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambayo ipo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ili iwe chini ya Manispaa.
Manispaa hiyo hadi sasa haina Hospitali  tangia ilipoanzishwa rasmi mwaka jana na imekuwa ikitumia kituo cha Afya  Mwangaza kuwa ndio kinatumika kama Hospitali yao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa