Home » » HATARI: AMNYIMA CHAKULA, MATIBABU, HYUDUMA ZA SHULE , KUMNYANYASA KISHA KUMFUKUZA NYUMBANI MTOTO WAKE WA KUMZAA

HATARI: AMNYIMA CHAKULA, MATIBABU, HYUDUMA ZA SHULE , KUMNYANYASA KISHA KUMFUKUZA NYUMBANI MTOTO WAKE WA KUMZAA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter Mguluchuma
  Katavi yetu blog
tuhuma kumtesa na kumnyanyasa kwa kumnyima chakula, matibabu  na huduma za  shule na kisha kumfukuza nyumbani kwake kwa kushirikiana na mama yake wa kambo kumnyanyasa  mtoto wake  aitwae Adamu Ramadhani (17)  wanafunzi wa kidato c ya Sekondari ya Kashaulili.
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri  Kidavashari aliwaambia jana wandishi wa habari kuwa mtuhumiwa alikamatwa hivi karibuni .
Alisema  Jeshi la Polisi  lilipata  taarifa  kutoka kwa  mtoto  huyo  kuwa  baba yake mzazi  anamfanyia   vitendo  vya ukatili  wa kijinsia  akiwa anashilikiana  na mama yake wakambo  aitwaye Joice Sina.
Kamanda Kidavashari  alieleza kuwa  manyanyaso na ukatili kwa mtoto huyo  hivi karibuni baada ya mama yake mzazi  kufariki  Dunia .
Kabla ya kifo cha mama mzazi wa mtoto  huyo   walikuwa wakiishi vizuri na kumpa huduma zote muhimu za msingi  za kibinadamu,
Kidavashari aliwaeleza waandishi wa Habari  ghafla hari ilibadilika  ikawa mtoto huyo  hapatiwi  mahitaji ya chakula  na wakati akiugua hapatiwi matibabu  chakula  na mahitaji yake ya shele
Na wazazi wake  waliamua kumfukuza nyumbani  na  walimtishia kuwa  wasimwone anakanyaga  nyumbani kwao atafute sehemu nyingine ya kuishi .
 Alisema  baada ya jeshi la polisi kupata malalamiko kutoka  kwa mtoto huyo  mwalimwa walimwandikia   baba yake  hati ya wito  ya mkutaka afike kituo cha Polisi  cha Wilaya ya Mpanda.
 Na alifika  kituoni hapo na kutoka kujihami  kwa kufungua taarifa kuwa amepotelewa na mtoto wake ambae ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kashaulili na ndipo alipokamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi .
Kamanda Kidavashari alisema   mtuhumiwa  atafikishwa Mahakamani  mara baada ya uchunguzi kukamilika  na ili aweze kujibu shitaka la kushindwa  kutoa huduma  mahitaji ya maisha  kwa mtoto  wake aliye chini ya uangalizi wake  na pia jitihada  zinafanyika  mke wake Joice  Sino ilinae aweze kufunguliwa mashitaka kama hayo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa