Home » » HOT NEWS: DC MPANDA ATOA AGIZO LA KUKAMATWA KWA VIONGOZI WA KIJIJI KWA KUUZA ADRHI

HOT NEWS: DC MPANDA ATOA AGIZO LA KUKAMATWA KWA VIONGOZI WA KIJIJI KWA KUUZA ADRHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza  amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda  kuwakamata na kuwafikisha  Mahakamani   Mwenyekiti wa Kijiji cha Kapamsenga Tarafa ya Karema  John Kaleba na Afisa mtendaji wake  Michael  Shuka pamoja na wajumbe 19 wa Serikali ya Kijiji hicho kwa kitendo chao cha kuwauzia adhi watu 52 katika eneo la hifadhi ya msitu na mapito ya wanyama (Ushoroba)
Mwamlima alitowa agizo hilo hapo jana  wakati alipokuwa akitowa taarifa  ya tume ya uchunguzi  wa  migogoro ya ardhi  katika  vijiji vya  Kapamsenga ,Ikaka na Nkungu  mbele ya  wajumbe wa kamati ya ulinzi na Usalama  wa Wilaya ya Mpanda  ofisini kwake mjini hapa.
 Alisema  Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya Wilaya ya Mpanda  kupitia idara  ya Ardhi  na Mali asili  awakamate na kuwafikisha Mahakamani waliokuwa viongozi wa Kijiji hicho ambao wamemaliza muda wao mashitaka ya  uvunjifu  wa sheria ya  wanyama pori  ya mwaka 2004.
Hii  ni  kufuatia  uliokuwa  uongozi wa Kijiji cha  Kapalamsenga  kuamua  kuuza  eneo  la Lyamgoloka  kwa Wananchi wapatao 52  hapo mwaka 2013 kinyume na sheria za Nchi .
Mwamlima alimwagiza  mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mpanda(ocd) kutowa ushilikiano  wa kutosha  na kuhakikisha  watu hao  21 walioamua kuuza eneo  eneo tengefu  la ardhi  wanakamatwa  wakiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wao  John Kaleba na Michael Kishoka(VEO).
 Alisema  kwa kuwa  Serikali ya Kijiji  cha Kapalamsenga  ilifanya utapeli  wa kuwaibia wananchi hao 52 hivyo  Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda  aisimamie  Serikali  ya  Kijiji  ili  watu hao waliokuwa wameuziwa  mashamba  wapewe mashamba  kwenye eneo  lililotengwa  kwa shughuli za kilimo katika Kijiji hicho.
 Alifafanua  kuwa tume hiyo  ya kufutilia  migogoro ya ardhi iliundwa   kutokana na kuwepo kwa migogoro mikubwa  ya ardhi katika vijiji vya  Kapalamsenga, Ikaka na Nkungu-
 Alisema tume hiyo imebaini kuwa  kamati za ardhi  za Vijiji hugawa  ardhi  zaidi ya  mara moja  zaidi ya kiwango  cha  kisheria cha Ekari  hamsini  na  hata   bila  vikao vya kisheria  kufuatwa  hivyo kusababisha  migogoro.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa