Home » » DC MPANDA KUUNDA TUME YA KUCHUNGUZA MADAI YA WAKULIMA WA TUMBAKU

DC MPANDA KUUNDA TUME YA KUCHUNGUZA MADAI YA WAKULIMA WA TUMBAKU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Walter Mguluchuma
      Katavi yetu blog
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima  anatarajia kuunda tume ya  kuchunguza  madai ya wakulima wa Chama cha Msingi  cha Tumbaku cha Mpanda kati  wanao dai malipo yao ya pili ya mauzo ya Tumbaku .
Mwamlima  alitowa kauli hiyo  hapo juzi wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari juzi ofisini  kwake katika Mtaa wa Ilembo Mjini  hapa.
Alisema afisi yake imekuwa  ikipokea malalamiko ya  wakulima  wa Tumbaku wa chama cha Msingi  Mpanda Kati juu ya kutolipwa malipo yao ya pili ya mauzo yao ya  Tumbaku  ya msimu uliopita .
Alitaja malalamiko mengine ya wakulima hao kuwa wanakilalamikia Chama hicho  kuwa kinawakata fedha nyingi  kwenye  mauzo yao ya Tummbaku  kwa ajiri ya gharama za  upandaji wa miti  kiwango ambacho akina uhalisia  wa idadi ya miche ya miti wanayokuwa wamepewa  kupanda.
Mwamlima  alisema  Serikari inathamini sana vyama vya msingi  hivyo  hayuko tayari kuona Chama hicho cha Msingi cha Mpanda Kati kinakufa au kinagawanyika kwani lengo la Serikali ni kuona vyama vyenye nguvu.
 Alisema zao la Tumbaku  linamchango mkubwa sana  katika kuchangia  mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda.
 Alifafanua kuwa tume  hiyo ya uchunguzi atakayoiteuwa  itaanza kufanya kazi hiyo mapema wiki ijayo na itatokana na watu wa idara mbalimbali na vyombo vya usalama .
 Hivi karibuni Mkuu huyo wa Wilaya alimwagiza Afisa  ushirika  wa  Wilaya hiyo kuitisha mkutano  mkuu wa dharula kwa ajili ya kujadili  madai yao ya malipo ya pili ya mauzo yao ya Tumbaku hata hivyo mkutano huu  ulishindwa kumalizika  baada ya wakulima wa chama hicho kushindwa kufikia muafaka na viongozi wao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa