Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Uchaguzi
wa Udiwani wa Kata ya Magamba
Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi
ambao ulishindwa kufanyika
Oktoba 25 unatarajiwa kufanyika kesho huku ukiwa
unawahusisha wagombea wawili ambao ni
mtu na mtoto wake
Uchaguzi huo wa Udiwani wa Kata ya Magamba
uliharishwa na tume ya uchaguzi kufuatia
kukosekana kwa karatasi za
kupigia kura za nafasi ya udiwani wa Kata hiyo
Wagombea wa Udiwani wa Kata hiyo wanatoka
kwenye vyama vya Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA) na
Chama cha Mapinduzi (CCM)
Ambapo Chama cha Mapinduzi kimemsimamisha Philipo
Kalyalya Mpela ambae ni
baba wa mgombea wa nafasi hiyo ya
Udiwani Joseph Mpela
Kalyalya (CHADEMA)
Kutokana na nafasi
hiyo kugombewa na mtu na mtoto wake kupitia vyama
tofauti uchaguzi huo wa kesho
umezuia hisia kubwa
za wakazi wa Manispaa ya Mpanda
na Mkoa wa Katavi kwa ujumla wake
Kwa upande
wake Joseph
alisema kuwa yeye aliamua
kugombea udiwani baada
ya kuona baba yake
ameongoza kata hiyo kwa kipindi cha miaka 20 bila
kuwaachia watu wengine hivyo umefika
wakati wa Kata hiyo kuongozwa nay eye ambae ni kijana
Nae Katibu
Mwenezi wa CCM wa Mkoa wa Katavi Joseph
Makumbule alisema kuwa Chama chake kimejipanga kuhakikisha wanashinda kesho
kwani katika uchaguzi wa Oktoba 25
Chama hicho kiliweza kuchinda Kata
zote 14 za Manispaa ya
Mpanda hivyo wanataka kuendelea
na rekodi hiyo
Katibu wa CHADEMA
wa Mkoa wa Katavi
Alimasi Ntije alisema
wamejiandaa kushinda uchaguzi huo ili waweze kuwa na
mwakilishi mmoja wa udiwani
ambae atakuwa anaingia kwenye
Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Mpanda anae
toka kwenye chama chao
Manispaa ya Mpanda inajumla ya Kata
15 ambapo katika
uchaguzi uliofanyika hivi
karibuni CCM walipata ushindi
katika Kata hizo
zote
0 comments:
Post a Comment