Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mtu mmoja
aliyefahamika kwa Jina
la Chiza Lameck (23)
Mkazi wa Kijiji cha Mgansa Wilaya ya Mpanda Mkoani hapa
amekutwa akiwa ameuwawa na mwili
wake kutelekezwa shambani
katika kijiji cha jirani huku
mwili wake ukiwa umenyofolewa sehemu
zake za siri, vidole vinne vya mkono
na kunyolewa nywele upande mmoja wa
kichwa chake
Kamanda wa Polisi wa
Mkoa wa Katavi Dhahiri
Kidavashari aliwaambia Waandishi
wa Habari kuwa tukio
la mauwaji hayo lilitokea
hapo Novemba sita
katika Kijiji cha Ilangu
Alisema
kabla ya tukio hilo kutokea
marehemu katika uhai wake
alikuwa akisumbuliwa na
tatizo la ugonjwa wa akili
Alieleza
kuwa marehemu alitoweka nyumbani
kwake kuanzia tarehe
2 Novemba na
ndugu zake walimtafuta bila
mafanikio yoyote
Kidavashari
alisema ndugu wa Marehemu
walipata taarifa Novemba 6 kuwa mwili wa marehemu Chiza umeonekana ukiwa katika Kijiji cha
jirani cha Ilangu ukiwa umetelekezwa
kwenye shamba
Baada ya kuwa
wamepata taarifa hizo ndugu
wa marehemu walifika
kwenye eneo hilo na
walikuta mwili wa ndugu yao ukiwa umetelezwa shambani
Alisema
baada ya kuufanyia uchunguzi wa
awali walikuta mwili wa marehemu ukiwa na
mapungufu kadhaa kwani sehemu za siri za mwili wake zilikuwa
zimenyofolewa , vidole vyake
vinne vya mkono wa kushoto na kunyolewa
nywele sehemu moja ya upande wa
kichwa chake
Alieleza
uchunguzi wa awali onaonyesha kuwa chanzo
cha mauwaji hayo kilisababishwa na imani za ushirikina
Kidavashari
alieleza kuwa mpaka sasa
hakuna mtu wala watu
aliyekamatwa kuhusiana na tukio
la mauwaji hayo na jeshi
la Polisi kwa kushirikiana na Wananchi wanaendelea na msako wa kuwabaini waliohusika
na mauwaji hayo
0 comments:
Post a Comment