Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Waandishi wa
habari wametakiwa wafahamu
vyema wajibu misingi na mipaka
ya majukumu yao ya kiutendaji
na kitaaluma kwa kila siku
Hayo
yalisemwa hapo jana na Katibu
Tawala wa Mkoa wa Katavi Mwandisi
Emanuel Kalobelo wakati akifungua
mkutano wa wadau wa habari wa Mkoa wa
Katavi katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mtakatifu Maria mjini Mpanda
mkutano huo uliandaliwa na Chama cha Waandishi wa habari cha Mkoa wa Katavi(KPC)
Alisema waandishi wa habari wanahitajika
kubeba dhamana ya uwajibikaji
bora tena uliotukuka kwa kutenda
haki na kuwa wazi
sana katika shughuli zao za kila siku
za kupasha habari na kuelimisha
jamii na katika nyakati za uchaguzi
Mwandisi Kalobelo
alieleza vyombo vya habari vinatakiwa kuwa huru
na kutekeleza majukumu yake
bila upendeleo na
kukandamiza ama kuumiza upande mwingine
na huo ndio msingi wa
maadili ya kazi za wanaabari
Alifafanua kwamba
kutokana na unyeti wa shughuli za uchaguzi
kipindi cha uchaguzi waandishi
wa habari wanatakiwa kuongeza umakini
maradufu katika utendaji wao wa
kazi ili kuisaidia jamii na Taifa kwa ujumla
kuchunga na kulinda na kuhifadhi
amani ya nchi isitetereke
Alisema waandishi wa habari wanapoandika habari za upande mmoja na kupendelea kwa kukandamiza upande mwingine wanakuwa hawatoi nafasi
kwa upande wa pili kwa
kutosiliza maoni yao
jambo hilo ni baya na ni kiashiria
tosha cha uvunjifu wa amani
Wananchi wanavipenda na
kuviamini sana vyombo vya habari pale vinapojitahidi kufanya kazi zao kwa umakini ,uwazi na tena
bila kuegemea upande wowote alisema Mwandisi Kalobelo
Hivyo vyombo vya habari vinatakiwa
vibebe pia wajibu wa kuunganisha jamii na sio
kuifarakanisha kwa sababu ya kutumiwa na
vyombo vyama vya siasa ama watu binafsi kwa
maslahi yao
Kwa upande wake
afisa wa kutoka TAKUKURU Mkoani
Katavi Simon Buchwa
alisema kuwa waandishi wa habari
wanawajibu wa kufanya kazi kwa
kuzingatia maadili yao
Alisema wapo
baadhi ya waandishi wa habari wamekuwa wakipokea rushwa ili kuwaandika kuwachafua watu na wengine kuwaandika vizuri hilo ni kosa
0 comments:
Post a Comment