Home » » MGOMBEA UBUNGE AKAMATWA NA POLISI KWA KUANDAMANA BILA KIBALI

MGOMBEA UBUNGE AKAMATWA NA POLISI KWA KUANDAMANA BILA KIBALI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mpanda Mjini (CHADEMA) Jonas  Kalinde amekamatwa akiwa na wafuasi kumi wa chama hicho  kwa tuhuma za  kufanya maandamano bila kibali
 Kalinde na wafuasi hao walikamatwa hapo jana  majira ya saa kumi na mbili na nusu  jioni katika  eneo la  mtaa wa Majengo A Mjini  hapa
 Mgombea huyo  alikamatwa wakati  akiwa  anatokea kwenye mkutano wa kampeni za ubunge wa jimbo la Mpanda  mjini uliofanyika  katika mtaa wa Kigamboni  Kata ya Shanwe
Wanadaiwa mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni mgombea huyo na wafuasi wa  Chama  hiyo walianza kutembea kwa miguu kwa lengo  la kwenda  kwenye ofisi za Chadema  zilizoko katika mtaa wa Majengo
 Wakati wakiwa njia  walipofika  eneo la Posta  walikamatwa na  polisi  na walipelekwa kituo cha  polisi  cha  Mpanda mjini kwa ajiri ya mahojiano
Kwa upande wake Jonas Kalinde alisema kuwa alilazimika  kutembea kwa miguu yeye na wafuasi wake  mara baada ya kumalizika kwa mkutano kutokana na gari anayoitumia kulete  hitilafu
 A lisema  baada ya  kukamatwa walifikishwa kituo  cha polisi ambako walikaa mpaka saa tatu na  nusu ndipo waliweza kupatiwa mdhamana na kuambiwa  kesho arudi tena
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri  Kidavashari  alithibitisha  kukamatwa kwa mgombea ubunge huyo 
Pia amewataka viongozi wa  vyama vya siasa  kufuata  sheria  na  taratibu zilizowekwa na  tume ya uchaguzi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa