Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mgombea Ubunge wa
Jimbo la Mpanda Mjini (CHADEMA) Jonas Kalinde ameitaka
Wizara ya Elimu iboreshe
mitaala yake kwa
kuanza kufundisha somo la elimu ya
uzazi wa mpango mashuleni na
kwenye vyuo mbalimbali
Kauli hiyo
aliitowa hapo jana mbele ya waandishi wa
habari katika Ukumbi wa White Club Mjini
Mpanda
Kalinde
alisema Wanawake wengi hawana elimu
ya kutosha ya uzazi wa
mpango suala ambalo linasababisha mimba
na zisizotarajiwa na vifo kutokana
na Wanawake kutofahamu toka mapema uzazi
wa mpango
Alisema huduma huduma
za uzazi wa Mpango na huduma za afya kwa akina mama na watoto
wachanga ni muhimu
sana zikatolewa bure nchi
nzima kuanzia Mijini , Vijijini na hata kwenye
taasisi za elimu ili
kuweza kupunguza vifo vya
akina mama wajawazito
na watoto wachanga
Alifafanua kuwa Serikali haina budi
kulipatia kipaumbele suala la uzazi wa mpango ili
kuwawezesha akina mama
wote kufikiwa na huduma hizi
nchi nzima
Hivyo alisema kuwa
endapo atachaguliwa kuwa Mbunge atahakikisha
elimu ya uzazi wa mpango inatolewa
mashuleni na vyuoni
kwa kutowa semina na
kusambaza vipeperushi
Pia
atapigania ongezeko la bajeti
ya Wizara ya afya hususani
katika uboreshaji wa huduma wa
huduma za uzazi
wa mpango pamoja na huduma ya
mama na mtoto mchanga
Vilevile atashirikiana na wadau mbalimbali
pamoja na AZAKI kuishawishi Serikali kuongeza bajeti kwenye ngazi ya Serikali kuu
na kwenye Halmashauri
Nae Galus Mgawe
Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo
la Mpanda Mjini kupitia ACT
Wazalendo alieleza kuwa wanawake
wengi na watoto wachanga hupoteza
maisha wakati wa kujifungua
kutokana na kukosa huduma sahihi za afya kabla
na baada ya kujifungua
Alisema
endapo atachaguliwa kuwa Mbunge
atatumia sehemu ya mshahara wake wa ubunge
pamoja na misaada ya
wafadhili katika kuboresha huduma za uzazi wa mpango na huduma
za mama na mtot o mchanga
Alieleza
kuwa atawasaidia wanafunzi wanaotoka
kwenye familia duni
misaada mbalimbali ili kupunguza
idadi ya wasichana wanaoacha
masomo kwa kukosa uwezo
fedha hili kupunguza
tatizo la mimba za utotoni
Alisema kitu cha msingi kwa yeye ni kuwa
na takwimu sahihi za hali
ya huduma za elimu ya uzazi
wa na elimu za
afya ya mama na mtoto za kila eneo la nchi na jimbo lake na
kuishawishi Wizara na Halmashauri kuongeza bajeti itakayotokana na mapungufu yatakayokuwa
yanajioonyesha kwenye takwimu
0 comments:
Post a Comment