Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mtu mmoja mkazi wa Kijiji cha
Ikingwamiza Kata ya
Mwamapuli Tarafa ya Mamba Wilaya ya
Mlele Mkoa wa Katavi ameuwawa kikatili
kwa kukatwa katwa na mapanga na watu
wasiojulikana wakati akiwa amelala nyumbani kwake usiku
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri
Kidavashari alimtaja mtu huyo aliyeuwawa kikatili kuwa ni Shija
Nkingo (60) Mkazi wa Kijiji
cha Ikingamiza Tarafa ya Mamba Wilaya ya
Mlele
Kidavashari
aliwaambia Wahandishi wa Habari kuwa tukio hilo la mauwaji ya kikatili lilitokea Septemba 10
mwaka huu majira ya saa saba usiku nyumbani kwake na marehemu Shija Nkingo
Alisema wauwaji hao ambao hawajafahamika siku
hiyo ya tukio walifika nyumbani kwa marehemu
majira ya saa saba usiku uku
wakiwa na mapanga na marungu
Alieleza baada ya kufika nyumbani kwa marehemu
wauwaji hao walivunja mlango wa nyumba
ya marehemu na kisha waliingia ndani ya
nyumba yake
Baada ya kuwa
wameingia ndani walimkuta marehemu akiwa
amelala na kisha walianza kumshambulia kwa kumkata kata kwa mapanga sehemu
mbalimbali za mwili wake mpaka kupelekea mauti yake
Kamanda Kidavashari alisema baada ya kufanya
mauwaji hayo ya kikatili wauwaji hau walitokomea mahari kusiko julikana na majirani walifika kwenye eneo hilo na
kukuta mwili wa marehemu ukiwa chini ya kitanda huku ukiwa umekatwa katwa
vibaya kwenye sehemu mbali mbali za mwili wake
Alisema chanzo cha mauwaji hayo bado haki
fahamika mpaka sasa na hakuna watu waliokamatwa kuhusiana na mauwaji
hayo
Kamanda
Kidavashari alieleza kuwa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na uongozi wa Kijiji cha Ikingwamiza wanaendelea
na uchunguzi ili kuwabaini watu
waliohusika ili waweze kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria
0 comments:
Post a Comment