Home » » KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA MANISPAA YA KWA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA MANISPAA YA KWA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Kiongozi wa  mbio za  Mwenge  Kitaifa  Juma  Khatibu  Chum  ameipongeza   Halmashauri ya Manispaa ya  Mpanda kwa kutekeleza agizo la Rais kwa  kujenga vyumba vya maabara  zilizokamilika
Chum alitowa pongezi hizo  hapo  jana  mara baada ya kufungua   majengo  matatu  ya maabara ya shule ya Sekondari ya Kashaulili  katika Manispaa ya Mpanda yaliojengwa na kukamilika huku yakiwa na vifaa vya maabara vilivyokamilika na  vimeanza kutumiwa na wanafunzi
 Alisema    anaipongeza  Manispaa ya  Mpanda kwa kutekeleza  agizo  la  Rais  kwani Halmashauri  nyingi  ambazo  mbio za  Mwenge  zimepita  wakekuta wamejenga  majengo  tuu  ambayo  hayaja kamilika kwa kuwa hayana vifaa vya maabara kama ilivyo Sekondari   hiyo ya Kata
 Amlipongeza pia  Mkurungezi wa  Manispaa hiyo  Selemani  Lukanga  kwa kuweza kusimamia na kufanikisha  ujenzi wa maabara  hizo  tatu za  sayansi
 Alisema  ukamilikaji wa  maabara  katika   shule za Sekondari  utasaidia  kupunguza tatizo la wataalamu  wa fani  mbalimbali hapa  Nchini  kwetu
Chum  alisema  kukamilika  kwa maabara hizo  tatu  leo hii  tayari wanafunzi wanao  soma kwenye  sekondari hiyo wameisha anza kunufaika
Alisema  bila  kuwepo na maabara katika  nchi   yetu  hatuwezi  kufikia  ulimwengu wa tatu  tunaohitaji kuufikia  ili  kuendana  na  mabadiliko ya  dunia
Mbio za  mwenge  wa Uhuru jana zilianza  mbio zake  katika  Manispaa ya  Mpanda na miradi 14 ilipitiwa na  Mwenge wa Uhuru  yenye  thamani ya jumla ya  Tsh1,364,224,845 nguvu ya wananchi ikiwa ni Tsh70,710,791, Halmashauri  Tsh 337,681,140  Serikali kuu  Tsh945,332,900 na wahisani walitowa  Tsh  10,500,000

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa