Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Baadhi ya Wananchi
wa Mtaa wa Kazima Wilaya ya Mpanda Mkoa
wa Katavi juzi katika hari isiyotarajiwa waliusimamisha msafara wa
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba
na maeneleo ya makazi
Angellah Kairuki wakitaka
kufahamu hatima ya fidia yao
ya ardhi yao ekari
500 zilichukuliwa na Halmshauri ya Mji wa Mpanda kwa ajiri ya ujenzi wa
chuo kikuu cha kilimo
Tukio hilo
la kusimamishwa kwa msafara huu wa Naibu
Waziri lilitokea hapo juzi majira ya saa tano asubuhi katika
eneo la mtaa wa Ilembo umbali wa kilometa tano kutoka Mpanda Mjini
Wananchi hao wa Mtaa wa
kazima wanaidai Halmashauri ya
Mji wa Mpanda kiasi cha shilingi milioni mia
nane kama fidia ya adhi yao
iliyochukuliwa na Halmashauri ya Mji wa Mpanda
toka mwaka 2011 kwa ajiri ya kupisha ujenzi wa chuo kikuu cha kilimo huko katika eneo la Kazima mjini Mpanda
Katika
tukio hilo wananchi hao walikuwa wamejipanga pembeni ya barabara wakiwa wanausubiri msafara wa Naibu Waziri
Kairuki uliokuwa umetokea kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa zilizopo kwenye mtaa wa Ilembo ambako alikuwa na kikao na viongozi wa Mkoa wa
Katavi ambao walikuwa wakimpatia taarifa
ya migogoro ya adhi ilipo katika Mkoa wa Katavi
Mara baada ya
kumaliza kikao chake na viongozi wa
Mkoa msafara huo ulianza safari ya kuelekea mjini Mpanda
ndipo baada ya muda mfupi baada ya kuanza msafara huo wananchi hao walisimamisha msafara huu hari
ambayo ilimlazima Naibu Waziri
aweze kusimama
Baada ya
kusimama Naibu Waziri
Kairuki alishuka kwenye gari lake
na kisha alisikiliza kero yao na aliwaahidi kurudi tena Mkoani Katavi
hapo mwezi Agosti na ndipo
atakuwa na muda mzuri zaidi wakuongea na
Wananchi hao hari ambayo iliwafanya
wananchi hao walidhike na kauli hiyo na kisha msafara huu uliendelea
Awali
kabla ya tukio hilo katika kikao
kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa
Mkoa wa Katavi baina ya waziri Kairuki na viongozi wa Mkoa wa Katavi alisema kuwa
madai ya fidia ya ardhi kwa wananchi wa hao yamekuwa ni ya muda mrefu hivyo wananchi hao wanatakiwa walipwe fidia yao mapema
Alisema
wananchi hao waliwahi kufika
mpaka ofisini kwake Mjini Dodoma na kumfikishia malalamiko hayo ya
kuchelewa kulipwa fidia yao ya shilingi milioni mia nane
Aliziagiza Halmashauri zote hapa Nchini
kutenga fedha za kuwalipa
wananchi fidia ya adhi kabla ya kuchukua kwanza adhi wa wananchi
wanapaswa wawe wanalipwa kwanza na pia itasaidia kupunguza kero kwa wananchi
kudai fidia zao
Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Mji wa Mpanda alimuhakikishia Naibu Waziri kuwa swala la wananchi hao analishughulikia kwani hata yeye
alilikuta toka miaka miwili
iliyopita alipo hamishiwa kwenye Halmashauri hiyo
Hata hivyo Lukanga alipoulizwa kama hati ya kiwanja
hicho Halmashauri inayo alijibu kuwa Halmashauri inayo kopi ya hati ya kiwanja
hicho na alipotakiwa aeleze hati yenye
ipo wapi katika hari ya kushangaza
alijibu kuwa hati hiyo imewekwa Bank na
ilipekwa na baadhi wajumbe wa bodi waliokuwepo
Baada ya majibu hayo Naibu Waziri aliagiza hati hiyo
ifatiliwe huko iliko wekwa Bank wa kuwa
haiku pelekwa bank wa kufuata
utaratibu na upo uwezekana hati hiyo
ikatumiwa na watu kwa manufaa yao binafsi
0 comments:
Post a Comment