Home » » MEMBE ATAKAE SHINDWA KURA AKIKATA RUFAA NI SAWA NA KENGE

MEMBE ATAKAE SHINDWA KURA AKIKATA RUFAA NI SAWA NA KENGE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Waziri wa mambo ya  Nchi za nje  wa Tanzania Benard  Membe  anayeomba  ridhaa  ya kuteuliwa  kugombea  Urais  na   Chama  cha  Mapinduzi (CCM)  anasema  mgombea yoyote wa nafasi  hiyo aliyeomba  ridhaa ya kuteuliwa  akishindwa  kushinda kwenye   Halmashauri kuu ya Taifa au kwenye Mkutano mkuu asipo kubali matokeo yakushindwa  mtu huyo anamfananisha na Kenge
 Membe  alitowa  hiyo  mjini  Mpanda   hapo jana  nje  ofisi  za  CCM Wilaya  ya  Mpanda  mara  wakati alipokuwa akiwahutubia  wanachama wa CCM na Wananchi wa Mji wa  Mpanda  mara baada ya kudhaminiwa na  wanachama  225  fomu za kuomba  ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea urais kupitia CCM
 Alisema  chama cha mapinduzi kimekuwa na utaratibu wa wagombea wake wanao  wania   Urais  kukubali matokeo pindi wanapo kuwa wameshindwa  hivyo hata wa waliomba ridhaa mwaka huu ya kuomba kuteuliwa na CCM   atakae shindwa  anapaswa akubali matokea  mgombea ambae atashindwa kwenye kura kwenye  wa NEC na kwenye mkutano Mkuu wa CCM  akipinga matokeo hayo yeye Membe anamfananisha mtu huyo sawa  na  Kenge
 Alieleza  CCM  haijawahi kufanya makosa kwenye uteuzi wake wa  mgombea Urais  hivyo kwa  kwa mgombea  atakae  shindwa  lazima   akubali  matokeo  alirudia tena kauli  yake  anae pinga ni sawa na Kenge
Alisema  katika wagombea wote waliomba ridhaa ya  kuteuliwa na  CCM kugombea Urais  yeye mtu anae muogopa  kushindana nae ni  Mizengo Pinda peke yake  ambae ni Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muunganano
 Membe  alieleza  endapo  Pinda angekuwa  hayumo  katika watu waliomba  ridhaa ya kuteuliwa  kupitia CCM basi  moja kwa moja angekuwa yeye Membe   ndiye  angekuwa mshindi  na moja kwa moja angekuwa na uhakika wa kuteuliwa na chama chake kuwa mgombea Urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu wa mwezi oktoba  mwaka huu
  Alisema  katika wagombea wote waliomba ridhaa ya kuteuliwa na CCM kugombea Urais  hakuna mgombea aliye na sifa kama yeye  kwani   hakuna mgombea  ambae   anae   yajua mambo ya nchi za nje kama yeye na mambo ya ndani ya nchi kama Membe
 Waziri  Bebard  Membe  amepata jumla ya wanachama wa CCM 225 waliomdhamini  kwenye fomu za kuomba ridhaa kuteuliwa kugombea urais kupitia CCM baada ya kumaliza shuguli hiyo Waziri Membe alielekea Mkoani Rukwa  kuendelea na zoezi la kutafuta wadhamini

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa