Home » » NHC YAKAMILISHA UZEJENZI WA NYUMBA 70 ULIOGHARIMU TSH BILIONI MBILI

NHC YAKAMILISHA UZEJENZI WA NYUMBA 70 ULIOGHARIMU TSH BILIONI MBILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Shirika la Nyumba la  Taifa (NHC) limekamilisha ujenzi wa  mradi  wa nyumba   70 zilizopo katika  eneo la Ilembo  Wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi  zilizogharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili
 Hayo yalisemwa hapo jana na Meneja  wa shirika la  Nyumba la Taifa wa  Mikoa ya Katavi na Rukwa Neemia   Msigwa  wakati alipokuwa akitowa taarifa  ya ujenzi wa nyumba ya shirika iliyojengwa na inayoendelea kujengwa  katika Mikoa ya Katavi na Rukwa mbele ya Naibu Waziri wa Ardhi  Nyumba  na maendeleo ya Makazi  Angellah  Kairuki wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya ujenzi wa  nyumba za shirika hilo Mkoani Katavi
 Alisema  mradi wa ujenzi wa  nyumba   sabini  za makazi  zilizopo  katika eneo la mtaa wa Ilembo  kilimeta tano kutoka Mpanda mjini  ambao kwa sasa umekamilika  ulianza  kujengwa Desemba 2012 ambao kwa sasa umekamilika  mradi huo umegharimu  kiasi cha  Tsh Bilioni 2.1
Msigwa alieleza   nyumba hizo 70  tayari  NHC imepata  mnunuzi wa  kuzinunua  ambao ni  Halmashauri ya Mji wa Mpanda  ambao wako kwenye mchakato wa kupata fedha za mkopo za kununulia  nyumba hizo kwenye   mabenki rafiki
Alifafanua kwa upande  wa Mikoa ya Katavi na Rukwa  shirika  la NHC   lina jumla ya miradi  minne  ambapo miradi mitatu ipo katika Mkoa wa Katavi na  mradi mmoja   upo katika Mkoa wa Rukwa
 Aliitaja miradi hiyo   kuwa ni   mradi wa  jengo la kitega uchumi  Paradise  uliopo  mjini  Mpanda  mradi wa  nyumba 20  za  makazi  za gharama  nafuu Inyonga  uliopo  Halmashauri ya Wilaya ya  Mlele  Mkoani hapa  na mradi  wa nyumba  za makazi  za  gharama   ya kati  jangwani  Town House ulipo  manispaa ya Sumbawanga Rukwa
 Alisema mradi wa jengo la kitega uchumi  la Paradise  wa ghorofa nne utakaogharimu kiasi chashilingi bilioni  3.1 unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu mradi   wa Inyonga unatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 1.2 na utakamilika mwishoni mwa mwaka huu na  mradi wa jangwani Sumbawanga wa ghorofa moja  nao  utakamilika  mwishoni mwa mwaka huu
Kwa upande wake   Mkurugenzi  wa   utawala na  uendeshaji  wa Mikoa wa NHC  Raymond Ndolwa  alieleza kuwa shirika  hilo linatarajia kuanza ujenzi  wa nyumba za gharama nafuu na ndogo zaidi kuliko wanazo jenga sasa
Alisema lengo la shirika hilo kujenga   nyumba  kwenye mikoa mbalimbali  ni kusogeza maendelea  karibu zaidi na wananchi
Naibu Waziri wa  Ardhi  nyumba na Maendeleo  ya Makazi  Angellah Kairuki alieleza kuwa mpaka sasa  bado mahitaji ya nyumba za kuishi ni  chache hapa  nchini  kwa ajiri ya makazi ya kuishi watumishi
Alisema  hadi sasa   kuna upungufu wa nyumba milioni moja za kuishi watumishi hapa  nchini  na mahitaji ya nyumba  yatazidi kuongezeka siku hadi siku
 Aidha  alitowa wito kwa Halmashauri  zote hapa  nchini  ziendelee kutowa  viwanja  kwa  NHC   ili shirika hilo  liendelee kujenga nyumba  nyingi za kutosha kwenye maeneo mbalimbali
Naibu Waziri  pia alilita shirika la nyumba la Taifa kuhakikisha linaongeza kasi ya ujenzi wa   wa miradi yake ya nyumba ili iweze kumalizika kwa wakati ili kupunguza tatizo la uhaba wa nyumba za  makazi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa