Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Wakulima wa zao la Tumbaku wa Mkoa wa Katavi kupitia vyama vyao
vya ushirika vya msingi wanatarajia
kuzalisha na kuuza zaidi
ya kilo milioni 14 ambazo ni sawa
na zaidi ya tani elfu kumi na nne kwa msimu wa mwaka 2014 na 2015
Haya yalielezwa hapo jana na
wakulima wa Tumbaku wa Mkoa wa Katavi kwenye risala yao iliyosomwa na Selemani Kaitila kwa niaba ya mwenyekiti
wa chama kikuu cha ushirika wa wakulima wa Tumbaku wa Mkoa wa Katavi(LATCU LTD) wakati wa ufunguzi wa ununuzi wa zao la
Tumbaku kwa msimu wa mwaka 2014 na 2015 uliofanyika kwenye chama cha ushirika
cha msingi mbele ya mgeni Rasmi mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi
Kaitila alisema kuwa msimu wa kilimo wa mwaka 2014 na 2015 wakulima wa vyama vya ushirika vya msingi wanatarajia kuzalisha na kuuza tumbaku yenye
jumla ya kilo 14,187,690 ambazo ni sawa na tani
14,187.61 zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 48
Msimu wa mwaka uliopita wakulima wa tumbaku wa Mkoa wa Katavi
wanachama wa LATCU
walizalisha kilo 13,305,706 za
Tumbaku ambazo ni sawa na tani 13,305.71 zenye thamani ya dola za
Kimarekani dola 30,337,009.68 wastani
wa bei kwa kilo moja iliuzwa kwa wastini wa dola 2.28
Na
Halmashauri za Mkoa wa Katavi
zilipata ushuru wa uliotokana na
Tumbaku kwa msimu huo kiasi cha shilingi Bilioni mbili
mia nne na ishirini na mbili milioni
laki tisa na kumi na mbili na kumi na mbili elfu
Alisema zao la tumbaku limekuwa
likiendeshwa kwa mkataba kati ya wanunuzi na wakulima wa Tumbaku kwa Mkoa wa Katavi makampuni yanayo nunua Tumbaku ni mawili
ambayo ni Premium Active(T) na Tanzania
Leaf Tobacco company(TLTC)
Alifafanua jambo kubwa wanalojivunia wakulima wa Tumbaku
wa Mkoa wa Katavi katika biashara ya Tumbaku
ni kuweza kulipa madeni
ya pembejeo kwa asilimia mia moja
Msoma risala alieleza
kuwa katika kuhakikisha kilimo
cha Tumbaku kinakuwa endelevu katika Mkoa wa Katavi suala la utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti linapewa
uzito na umuhimu wa pekee
Alitaja
baadhi ya changamoto walionayo
wakulima wa Tumbaku ni utunzaji wa miti
iliyopandwa imekuwa ikiathiriwa
na uchomaji holela wa moto na uchungaji holela wa mifugo
Kwa upande wake
Mkuu wa Mkoa wa Katavi DR Ibrahimu
Msengi ambae alifungua msimu wa ununuzi wa zao la Tumbaku alisema kuwa
vyama vingi vya ushirika vya msingi
vimekuwa na migogoro kutoka na viongozi wanaoviongoza vyama hivyo kutokuwa
waaminifu
Alisema wakulima wa Tumbaku wanatakiwa kuwacha
kuwachagua viongozi wanao waongoza kwenye vyama vyao vya msingi wale ambao
wanajali masilahi ya wakulima na wale wenye upeo mkubwa ambao wanauwezo wa kuwatetea
wakulima kwenye masilahi yao
Chama
kikuu cha ushirika cha wakulima wa Tumbaku cha Mkoa wa Katavi LATCU
kinanawachama saba wa ushirika vya msingi ambavyo ni Nsimbo,
ukonongo, Katumba. Mishamo Tamcos, Kasokola,Amcos, Mpanda kati na
Ilunde
0 comments:
Post a Comment