Home » » BODA BODA CHANGAMKIENI KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA

BODA BODA CHANGAMKIENI KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na    Walter  Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza  Mwamlima awewataka Boda boda walioko katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa wa Katavi  wachangamkie kujiunga na  mfuko wa Bima ya afya NHIF   ili waze kupata tiba  ya uhakika
 Mwamlima alitowa kauli hiyo hapo jana wakati akiwahutubia wananchi wa Kata ya Mwamkulu wakati wa ziara yake ya kuwahamasisha  wananchi wa Halmashauri ya  Mji wa Mpanda wajiunge na mfuko wa NHIF katika ziara hiyo ambayo alikuwa amefuatana na viongozi wa mfuko wa bima ya afya wa Mkoa wa Katavi na Rukwa wakikuwa wameongozwa na meneja wa mfuko huu wa mikoa ya Rukwa na Katavi   Abdiel Mkayo
 Alisema  boda boda wamekuwa wakipata ajari mara kwa mara hivyo  wakijiunga na mfuko huo watakuwa na uhakika wa kupata matibabu  pindi  wanakuwa wamapata ajari
 Alisema sio muda wote  huwa wanakuwa na pesa za matibabu  hivyo endapo  watakuwa wamejuimga na mfuko  itakuwa kwao ni   rahisi kupatiwa huduma ya matibabu hata kama wanakupokuwa  hawana fedha
Kwa upande wake   Meneja wa  mfuko wa bima ya afya NHIF wa mikoa ya Rukwa na Katavi  Abdiel Mkayo  alisema kuwa  mfuko huo ni muhimu sana kwa watu ambao wanakuwa wamejiunga na mfuko kwani sio wakati wote mtu  anaweza kuwa na pesa
 Alisema  wako baadhi ya watu wamekuwa na hofu ya kujiunga na mfuko huu kutokana na kukosekana kwa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma
 Alifafanu  ukosefu huo wa dawa umekuwa ukichangiwa na ukosefu wa fedha  na kamati zinazokuwa zimechaguliwa kutosimamia ipasavyo  vituo vyao vya kutolea huduma
Nae  mratibu  wa   mfuko wa afya ya jamii Lesipita Kalugendo  aliwaeleza  kuwa  Halmashauri ya mji wa Mpanda imeisha jipanga ili kuhakikisha kila mtu aliyejiunga na mfuko huo  anapo kuwa inahitaji huduma ya dawa dawa hazikosekani zinakuwepo kwa pindi chote
 Alisema indapo mtu atakuwa ameandikiwa dawa na kukosekana kwenye zahanati na vituo vya afya mtu huyo atalazimika kwenda kwenye  hospitali teule ya Halmashauri ya mji wa Mpanda na kupatiwa huduma hiyo ya dawa au kwenye maduka maalumu ambayo yameteliwa kutowa huduma hiyo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa