Home » » DC MPANDA AWAAGIZA VIONGOZI KWENDA KILA MTAA NA KILA NYUMBA KUHAMASISHA WATUWAJIUNGE NA MFUKO WA ( NHIF)

DC MPANDA AWAAGIZA VIONGOZI KWENDA KILA MTAA NA KILA NYUMBA KUHAMASISHA WATUWAJIUNGE NA MFUKO WA ( NHIF)

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza  Mwamlima  amewaagiza viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda wahakikishe wanakwenda kwenye  mtaa kwa mtaa  na nyumba kwa nyumba kuwaelimisha watu wajiunge na mfuko wa bima ya Afya ya (NHIF)
 Mwamlima  alitowa agizo hilo hapo juzi wakati wa uzinduzi wa   huduma ya matibabu   ya njia ya kadi (tika ) uzinduzi uliofanyika  katika viwanja  vya shule ya msingi Kakese
 Alisema   kutokana na umuhimu wa huduma ya mfuko huo ni vema viongozi wakaacha kukaa ofisi na waende  kila mtaa kwa mtaa na kuwaelimisha  watu umuhimu wa kujiunga na mfuko huo
 Alifafanua kuwa hakuna  nchi yoyote hapa   duniani ambayo wananchi wake hawachangie  hata  kidogo  kwenye  Serikali   yao
 Alisema endapo  wananchi wataelimishwa  umuhimu  wa kuchangia  mfuko wa tiba kwa njia ya kadi(TIKA) itawasaidia  kwa ajiri ya maendeleo ya afya zao
Awali kabla ya uzinduzi wa huduma ya  uzinduzi huo na uzinduzi wa   bodi ya mfuko wa  bodi ya afya ya Halmashauri ya mji wa Mpanda  Meneja wa   NHIF   wa Mikoa ya Rukwa na Katavi   Abdiel Mkayo alieleza kuwa hari ya uchangiaji kwa wananchi katika mfuko  wa afya  wa afya kwa jamii  tiba kwa kadi  sio ya kulidhisha na Mkoa wa katavi uko nyuma
 Alisema kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda  ni watu  1147 tuu wanachangia mfuko huo ambao ni sawa na asilimia tatu na Halmashauri ya Wilaya ya Mlele inao wachangiaji  1,184 ambao ni sawa na asilimia tano
 Mkayo  alieleza kuwa kwa upande wa Halmashauri ya Nsimbo  ina jumla ya kaya  elfu kumi na moja ambazo zinachangia mfuko huo sawa na asilimia orobaini na saba
 Alifafanua kuwa hadi kufikia Desemba mwaka huu Serikali imepanga  wananchi asilimia 30 wawe wamejuunga na mfuko huu na  wawe wanapatiwa matibabu kwa njia ya matibabu kwa njia ya kadi
 Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Mji wa Mpanda Selemani Lukanga  alieleza kuwa  wananchi waachane na mawazo ya kudhani kwamba mfuko wa bima ya afya upo kwa ajiri  ya watumishi tuu
 Hivyo katika swala la afya watumishi hawaguswi peke yao  kwa hari hiyo wananchi wanao wajibu wa kujiunga na mfuko wa bima  ya afya  kwakuwa  hakuna wananchi ambae haitaji huduma ya afya
 Nae mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Enock Gwambasa alieleza kuwa mwitikio wa  wanachi   kujiunga na mfuko huu  ni mdogo sana  kutokana na watu kuwasikiliza  watu ambao sio wataalamu
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya mfuko wa afya   wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda  Fotunata Issaya aliwataka wananchi wa Halmashauri hiyo kujiunga na mfuko wa bima ya Afya
Alisema  watu ambao watajiunga na mfuko huo watapata matibabu ni sawa na bure kwani kiwango wanacho changia cha shilingi elfu kumi kwa mwaka ni sawa na kupatiwa matibabu bure

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa