Home » » HATARI SANA: MWANAMKE AUAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA VISU TUMBONI NA SEHEMU ZA BEGA LAKE NA WATU WASIOFAHAMIKA.

HATARI SANA: MWANAMKE AUAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA VISU TUMBONI NA SEHEMU ZA BEGA LAKE NA WATU WASIOFAHAMIKA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mwanamke  mmoja aliyejulikana kwa jina la  Vestina   Peter(27)  Mkazi wa Kijiji   cha Ilalangulu Tarafa ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele  Mkoa wa Katavi  amekutwa akiwa ameuwawa  kikatili kwa kuchomwa  na visu   tumboni hadi utumbo wake kutoka nje  na kwenye sehemu  ya bega lake na watu wasiofahamika 

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari  aliwaambia waandishi wa habari kuwa tukio hilo la mauwaji ya kikatili lilitokea hapo juzi majira ya saa kumi na mbili jioni
 Alisema kabla ya tukio hilo marehemu aliaga nyumbani kwake alikokuwa akiishi na mumewe   kuwa anakwenda shambani kwake kuimbua mahindi katika eneo la  Kazaroho 

Kidavashari alieleza  baada ya marehemu  kuelekea huko shambani hakuweza  kurudi nyumbani kwake kwa muda wa siku mbili  hadi  hapo juzi  mwili wake ulipo onekana  ukiwa shambani kwake huku ukiwa  amechomwa vifu tumboni hadi utumbo wake kutoka nje  na  akiwa na majeraha ya kuchomwa na vifu sehemu ya  kulia ya bega lake 

 Alisema  baada ya mwili wa marehemu huyo  kupatikani   taarifa zilitolewa kwenye kituo cha Polisi cha kibaoni ambao walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi  na  chanzo cha mauwaji ya kikatili ya mwanamke huyo  bado hakifahamika.

Kamanda wa Polisi Kidavashari  alieleza   mpaka sasa  jeshi la   linawashikilia watu  watu wawili   kwa mahojiano zaidi  ambao ni   Charles  Julio(42)  Mkazi wa Ilembo  na  Fred Ndaina (42) Mkazi wa Kijiji cha Ilalangulu Kata ya Kibaoni.

Alisema  watuhuwa hao wanatarajiwa kufikishwa  mahakamani   mara baada ya uchunguzi  utakapo kuwa umekamilika ili wakajibu tuhuma zinazo wakabili

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa