Home » » WATATU WAWAONESHA NIA YA KUGOMBEA JIMBO LA MPANDA MJINI LINALO ONGOZWA NA ARFI

WATATU WAWAONESHA NIA YA KUGOMBEA JIMBO LA MPANDA MJINI LINALO ONGOZWA NA ARFI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Watu watatu wameonyesha nia ya kugombea ubunge wa Jimbo la Mpanda Mjini   Mkoa wa Katavi (CCM) jimbo ambalo linaongozwa na Mbunge Said Arfi (CHADEMA) aliyeliongoza jimbo  hilo kwa kipindi cha miaka kumi sasa
Wanachama hao walioanza harakati  za kugombea jimbo hilo ni  Gabriel  Mnyele  ambae  ni mwanasheria maarufu wa  jijini  Dares salaam  anaejishughulisha  na kazi ya uwakili  wa kuwashauri watu binafsi  na makampuni  mambo ya kisheria
Mwingine ni Sebastiani  Kapufi ambae aliwahi kuwa  Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mpanda kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia  mwaka 2007  hadi   mwaka 2012 na pia aliwahi kuwa Mwenyekiti  wa Halmashauri  ya Wilaya ya Mpanda  kwa kipindi cha miaka mitano
 Na  Galus  Mgawe  ambae kwa sasa  ni meneja wa kampuni ya  Aitel  wa Mikoa ya Mtwara , Songea na Lindi
Wagombea wawili  Galus  Mgawe na Sebastiani Kapufi  hii itakuwa ni kipindi chao cha tatu kushiliki  kwenye kinyang’ilo  cha kugombea  ubunge  kwenye kura za maoni  za CCM
Uchaguzi  Mkuu uliopita  wa mwaka 2010 CCM walimsimisha  kugombea  ubunge wa jimbo hilo Sebastiani Kapufi ambae  alishindwa na  mbunge wa sasa Said Arfi (CHADEMA)
Jimbo la Mpanda  mjini  lilikuwa halijawahi kuongozwa na mbunge aliyeongoza jimbo hilo kwa vipindi viwili isipo kuwa Mbunge alipo  sasa  ndiye aliyeweza kuongoza jimbo hilo ambalo  lipo hati hati kurudi CCM kutokana na mgawanyiko ulipo sasa  ndani ya CHADEMA katika jimbo la Mpanda Mjini

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa