Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la Mwita
Paulo (Ryoba) 25 mwalimu wa Shule
ya Msingi Lukama Makazi ya Wakimbizi ya Katumba
Mkoa wa Katavi ameuwawa kikatili
kwa kuchomwa na vifu kifuani na watu wasio julikana
Tukio la mauwaji hayo ya kikatili ya mwalimu huyo lilitokea hapo juzi
majira ya ya saa mbili na
nusu usiku katika
eneo la shule ya msingi Mpanda
katika mtaa wa Mpanda Hotel mjini
hapa
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa habari kuwa
marehemu kabla ya kifo chake
hicho aliaga kwenye kituo chake cha kazi katika shule ya Msingi Lukama kuwa anakwenda mjini Mpanda katika shule ya Sekondari ya Mwangaza kufanya
mtihani wa kidato cha sita
Alisema marehemu alikuwa amefuatana na waalimu wenzake ambao wanafundisha shule za msingi mbalimbali zilizoko kwenye makazi
hayo ya Wakimbizi ya Katumba ambao nao walikuwa wanakwenda kufanya mtihani wa
kidato cha sita kwenye kituo cha kufanyia mtihani katika shule ya Sekondari ya Mwangaza
Kidavashari
alieleza marehemu akiwa na
waalimu hao aliweza kufika katika shule ya mwangaza na
kufanya mitihani yake ambapo alikuwa
akirudia kufanya mtihani ya baadhi ya
masomo ambayo hakuwa amefanya vizuri katika masomo yake ya kumaliza kidato cha sita
Baada ya kumaliza mitihani waalimu wenzake walianza safari la kurejea kwenye vituo vyao
vya kazi katika makazi ya wakimbizi ya
Katumba lakini yeye aliamua kubaki mjini
Mpanda
Alisema
baada ya hapo marehemu Mwita Paulo
hakuonekana tena mpaka mwili wake ulupoonekana
katika eneo la shule ya Msinngi
Mpanda mtaa wa Mpanda Hotel huku ukiwa
amechomwa vifu katika sehemu zake
za kifuani
Kamanda
Kidavashari alisema chanzo cha tukio hilo bado hakija fahamika na hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusiana
na tukio hilo na polisi wanaendelea
na uchunguzi wa kifo cha mwalimu huyo
0 comments:
Post a Comment