Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi wameelezwa
kuwa majukumu makubwa ya TAKUKURU
ni kuzuia rushwa na
kutowa elimu kwa wananchi juu ya rushwa
na kupambana na rushwa
Hayo yalisemwa
hivi karibuni hivi na Mratibu wa dawati la
elimu kwa umma wa TAKUKURU wa Mkoa wa Katavi Everist Ndongolo kwenye semina ya waandishi wa Habari wa
Mkoa wa Katavi iliyoandaliwa na TAKUKURU
Mkoa wa Katavi iliofanyika katika ukumbi
wa jengo la Ofisi ta Takukuru Mjini hapa
Ndogolo
alieleza kuwa TAKUKURU imeandaa semina hiyo ya siku moja kwa lengo
kueleza jitihada zinazofanywa na
Serikali kuhusu mapambano dhidi
ya Rushwa
Alisema majukumu
makubwa ya TAKUKURU ni kufanya
kazi ya kuzuia rushwa , kutoa elimu juu
ya rushwa na kupambana na Rushwa
Alifafanua kuwa katika kuzuia rushwa kunahusisha utafiti na katika kutoa elimu kunahusisha
mikutano ya hadhara na
kupitia club za
shule na vyuo
Ndogolo alieleza kuwa zipo aina kuu mbili za rushwa
ambazo alizitaja kuwa kuna rushwa
kubwa na rushwa ndogo
Alisema rushwa ndogo huwa zinawagusa watu au mtu mmoja mmoja pamoja na viongozi wa ngazi ya chini na Rushwa kubwa inawgusa viongozi wa wakubwa
Alitaja baadhi ya sababu zinazopelekea
kuwepo kwa rushwa katika jamii kuwa ni kupanda kwa gharama za maisha ,sheria zilizopitwa na wakati pamoja na mazoea waliyojizoweshea wananchi
kwa watumishi kwamba bila kutoa chochote hawezi kutimiziwa kile ambacho
anakihitaji
Nae Mkuu wa
TAKUKURU wa Mkoa wa Katavi Cristopher Nakua alisema kuwa taasisi hiyo ya kuzuia na kumbambana na rushwa
imekuwa ikikutana na changamoto
mbalimbali
Nakua alitaja baadhi ya changamoto
kuwa ni wananchi kutotowa na ushilikiano wa kutosha kwa TAKUKURU hali
ambayo imekuwa ikirudisha
nyuma ufanisi wa utatuzi
wa masuala ya Rushwa
Mkuu huyo wa
TAKUKURU wa Mkoa wa Katavi alitowa
wito kwa wananchi wa Mkoa wa
Katavi viashiria vya kuwafichua au kutoa taarifa zinazoleta
viashiria vya Rushwa katika
sehemu mbalimbali na katika sehemu zao za kazi
0 comments:
Post a Comment