Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi linamshikilia mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Mazigo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za
kumkamata na silaha bunduki ya kivita
aina ya AK 47 na Gobore moja
Mtuhumiwa huyo
aliyekamatwa ametajwa kuwa ni
Emanuel Herman (KAMTUPE) 36 ambae
ni mkazi wa Kijiji cha Masigo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoani hapa
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema kuwa tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na
silaha hizo mbili lilitokea hapo juzi majira ya
saa nane usiku katika Kijiji hicho cha Masigo
Kidavashari
alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa
kufuatia taarifa za kutoka kwa raia wema walilizozitowa kwa askari wa wanyama
poli kuwa mtuhumiwahuyo amekuwa akimiliki
silaha kinyume cha sheria na amekuwa akizitumia kwa uwindaji haramu
Baada ya taarifa
hizo kuwafikia askari wa wanyama
poli walianza msako wa kumsaka mtuhumiwa
huku wakiwa wanaongozwa na Afisa wa wanyama pori Cedrick
Mashauri
Kidavashari alieleza katika
msako wa askari wa wanyama
poli hao walifanikiwa hapo juzi
kumkamata mtuhumiwa Emanuel Herman(KAMTUPE) akiwa silaha bunduki mbili
moja aina ya AK 47 na
nyingine aina ya Gobore
Alisema mtuhumiwa alikuwa akimiliki bunduki hizo
kinyume cha sheria na alikuwa
akizitumia kwa ajiri ya uwindaji haramu
katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi na kwenye mapori ya akiba
Mtuhumiwa bado
anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi na anatarajiwa kufikiwa mahakamani
mara baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika aliwaambia waandishi wa habari Kamanda
Kidavashari
Hivi karibuni Askari wa Hifadhi ya Taifa ya
Katavi waliweza kufanya doria na
kufanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na vipande vitatu vya meno ya
Tembo yenye thamani ya zaidi ya shilingi
milioni 11 ambayo walikuwa wakitaka kuyasafirisha kutoka kwenye Makazi ya Katumba Wilaya ya Mlele kuyapeleka
Mkoa wa Tabora
0 comments:
Post a Comment