Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi linawashikilia watu watu wawili wakazi wa Kijiji cha
Masigo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya
Mlele kwa tuhuma ya kuwakamata na
nyama ya kiboko zaidi ya kilogramu 50 katika matukio mawili tofauti
Watuhumiwa hao
waliokamatwa wametajwa kuwa ni Ramadhan
Majengo(66) Emanuel Herman(36)wote wakazi wa Kijiji cha Mazigo
Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa
tukio la kwanza la kukamatwa kwa
watuhumiwa hao wawili wakiwa na
nyama ya kiboko lilitokea hapo juzi
Katika tukio hilo
ambalo lilitokea majira ya saa sita na
nusu askari wa Wanyama pori ambao waliokuwa doria wakiongozwa
na Askari mwenzao Cedrick
Mashauri walimkamata mtuhimwa Ramadhani
Majengo akiwa na nyama ya Kiboko
kilo 40 akiwa nyumbani kwenye Kijiji cha Mazigo
Kamanda
Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari kuwa
mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa za kutoka kwa raia wema ambao
walitowa taarifa kwa askari wa wanyama poli kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akijihusisha na
uwindaji haramu wa wanyama kwenye Hifadhi ya Taifa ya Katavi na kwenye mapori
ya akiba
Alisema tukio la
pili la kukamatwa kwa watuhumiwa hao lilitokea hapo jana majira ya saa saba usiku huko katika eneo la Kijiji
cha Mazigo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya
Mlele
Katika tukio hilo A skari wa Wanyama poli
ambao walikuwa wakifanya dolia walimkamata mtuhumiwa Emanuel
Herman akiwa na nyama ya Kiboko kilogramu 15 ambazo zilikuwa zimebanikwa
Kidavashari
alisema watuhumiwa hao wote wawili wanaendelea
kushikiliwa na jeshi la Polisi na wanatarajiwa kufikishwa
mahakamani mara baada ya uchunguzi
utakapo kuwa umekamilika
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi ametowa wito kwa Wananchi
wale ambao wanajihusisha na biashara
haramu ya nyara za Serikali waache
mara moja kwani kufanya hivyo ni
kinyume cha sheria na
zinasababisha hasara na uharibifu mkubwa wa rasilimali
za Taifa
0 comments:
Post a Comment