Na
Walter Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi linamshikilia Deocratias Pastory (30)
Mkazi wa Kijiji cha Ntumba Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma
za kumjeruhi vibaya tumboni kwa kumkata na panga hadi utumbo kutoka
nje Masanga Elias(28) Mkazi wa Kijiji cha Stalike
Tarafa ya Nsimbo baada ya kumfumania akifanya mapenzi (tendo la ndoa)
jikoni na mke wake
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina msaidizi
mwandamizi Dhahiri Kidavashari aliwaeleza waandishi wa habari
ofisini kwake kuwa tukio hilo lilitokea hapo Machi
29 majira ya saa tano usiku katika Kijiji cha Kapanga
Wilaya ya Mpanda nyumbani kwa mtuhumiwa Deocratias
Kamanda
Kidavashari alisema siku hiyo ya tukio majira ya mchana
mtuhumiwa aliaga nyumbani kwake kuwa anaelekea
katika Kijiji cha Kapanga kwa ajiri ya shughuli
za shambakwa kutumia usafiri wake wa baiskeli
Alieleza
wakati akiwa njiaani akiendelea na safari yake baiskeli yake aliyokuwa
anaitumia iliharibika na hakuwa na namna yoyote ile ya kuitengeneza
Ndipo mtuhumiwa
alipoamua kuanza safari ya kurudi nyumbani ambapo aliweza kufika
nyumbani kwake walikokuwa wakiishi na mkewe muda wa saa tano usiku
Kidavashari
alisema baada ya kufika nyumbani alimkuta mke wake
aitwaye Tabu Nestory(20) akiwa anafanya mapenzi
(tendo la ndoa) jikoni na mtuhumiwa huku akimtamkia kuwa
anampenda sana
Alisema
kitendo hicho cha kumfumania mke wake akifanya tendo la ndoa na mtuhumiwa
huku mkewe akimwambia mtuhumiwa kuwa anampenda sana kilimkasilisha
sana mtuhumiwa Deocratius Pastory
Ambapo kitendo
hicho kilisababisha mtuhumiwa kuanza kumshambulia
Masaga Elias kwa kumkata na panga tumboni hadi utumbo kutoka
nje ambae muda huo alikuwa bado akiendeku kufanya tendo la ndoa
na huku mtuhumiwa akiwa na shuhudia
Alisema
kisha mtuhumiwa baada ya kuwa amemjuruhi vibaya mgoni wake alimkata
mkewe kwa panga kwenye mkono wake wa kushoto
hari ambayo ilimfanya mkewe apige kelele ya kuomba msaada kwa
majirani na majirani walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi
Kamanda
Kidavashari alisema mpaka sasa majeruhi
Deoctatius Elias bado amelazwa katika Hospitali ya
Wilaya ya Mpanda akiwa anaendelea kupatiwa matibabu haku hari yake ikiwa mbaya
Amewaasa
wanandoa wawe na tabia ya kuheshimiana na kufuata
maadili yanayokubalika na Dini na jamii ili kuepusha
migogoro ya nanma hii na pindi inapojitokeza wahusika
wajitahidi kutoa taarifa kwenye vyombo vya sheria ama
mamlaka zilizokasimishwa kusuruhisha migogoro ya
wanandoa badala ya kujichukulia sheria mikonon
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment